Zinazobamba

JUKWAA LA KATIBA :RAIS WANGU KIKWETE USIJIFICHE NYUMA YA HAO CCM, JITOKEZE UOKOE MABILIONI HAYA YA WALALAHOI

Kaimu mwenyekiti wa jukwaa la katibaBw. Hebron Mwakagenda Akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari huko ofisini kwake
Jukwaa la katiba Tanzania JUKATA limefanikiwa kupenya na kuingia katika bunge la katiba na kukutana na kamati zote kumi na mbili, ambapo katika kamati hizo wamebaini mapungufu makubwa ambayo yanatia shaka upatikanaji wa katiba mpya inayoendelea kujadiliwa huko mjini Dododma,

Akizungumza na mwandishi wa mtandao huu mapema hii leo,Kaimu mwenyekiti wa jukwaa la katiba Tanzania Bw. Hebron Mwakagenda, amsema katika safari yao hiyo wamebaini mambo makubwa kumi ambayo yanatia shaka kwa katiba mpya ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania kupatikana, 
Mwakagenda amesema kwanza kabisa achilia mbali idadi ya wabunge ambao hawajitia mguu katika bunge hilo toka kuanza kwa awamu ya pili ,lakini lokoo inaonyesha kuwa wabunge wengi hawahudhilii vikao vya kujadili rasmu ya katiba,
Amesema tokea kuanza kwa vikao hivyo, Wabunge wengi wamekuwa hawahudhulii vikao, kwa sababu hawahudhulii vikao basi kamati inaamua kufanya kikao hicho kama semina  ili waende kula kodi za watanzania bure huku wakijua wazi kufanya hivyo ni ubadhilifu wa mali ya umma,

Wamekuwa wakibali vikao kuwa semina hiyo ni kutokana na akidi kutotimia, sasa wanaamua kujitengenezea mazingira ili waendelee kupiga psa za walala hoi
Mwakagenda akifafanua jambo kwa waandishi wa habari mapema hii leo.

Katika hatua nyingine Mwakagenda ameibua ufisadi mwingin unaofanywa na mawaziri katika bunge hilo la katiba kwa kusema , mawazili hao wamekuwa wakijitengenezea mazingira ya kutohudhuria vikao lakini bado posho zao zikiendelea kumiminika katika akaunti zao
Mawaziri wanatakiwa kutoa taarifa kwa waziri mkuu juu ya udhulu wao, lakini wanapofanya hivyo bado fedha zao zinaendelea kuingia katika akaunti zao wakati wao wanafanya kazi tofauti na kutunga katiba, amesema ilie ni sehemu yao ya kazi kwa nini sasa bunge la katiba liwalipe pesa huku wakifanya kazi nyingine Alihoji
SABU TATU MUHIMU KIKWETE KUNUSURU MCHAKATO WA KATIBA
  1. Mahudhulio hafifu ya wajumbe wa bunge la katiba, hakuna wajumbee kiasi kwamba wachumia tumbo wachache wameamua kubadili vikao hivyo kuwa semina za kujipatia kipato,. LOkoo zinadaiwa kutotimia kwa kila kamati na hivyo wanaamua kubadili vikao kuwa semina za kujaziana uwezo, alipohojiwa na jukata, mwenyekiti wa bunge hilo alikili hadharani kuwa akidi hazitimiii
  2. Kukosekana kwa muafaka wa malidhiano, hii ni sababu muhimu sana kwani mpaka sasa kuna sauti nyingi toka kila kona ya nchii hii ikisema bunge hilo lisimame kwanza kwani kuna miradi mingi ya kufanya kwanza, mpaka sasa watu wengi hawaridhika na kuendelea kwa vikao vya tume hivyo, hivyo rasi anaombwa kuingilia mchakato kunusuru mabilioni ya walipa kodi,. Alipoulizwa na mwandishi wa mtandao huu kuhusu uweezo wa rais kuingilia kati mchakato, Mwakagenda alisema ni kweli rais hana mamlaka ya kuvunja bunge hilo lakini pia ni kweli kuwa rais hana malakaya kuanzisha mchakato wa kutunga katiba mpya, kwa sababu amelianzisha ni lazima basi busara zitumike pia kulimaliza,. Tunajua kuwa rais alikuwa na nia nzuri ya kutupatia katiba lakini kutokana na sababu ambazo hazizuiliki basi rais wtu kipenzi aangalienamna ya kutusaidia kuokoa mabilioni haya ya shilingi yanayotumika huku tukijua wazi kuwa katiba mpya haipatikaniki
kukosekana kwa theruthi mbili ya  wajumbe toka Zanzibar ili kupitisha katiba, Hili ni tatizo ambalo Samweli sita mwenyewe amekili kuwa hilo tatizo lipo na hana uhakika wa kupata hiyo 2/3 toka visiwani Zanzibar, watafiti wa mambo wanasema Wajumbe hao ndiyo moyo wa UKAWA.

JUKATA LATOA MSIMAMO WAKE
Jukata linataka mchakato wa katiba mpya usimame upishe michakato mingine ya kitaifa tena yenye uzito mkubwa kama wa uandikishaji wa vitambulisho vya kitaifa, uandikishaji wa wapika kura, kwenye daftari la kudumu la wapiga kura kwa mfumo wa kielectroniki (BVR),Uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu wa mwakati ambao miradi yote hiyo inahitaji pesa nyingi za kufanikisha kwake

No comments