TANROADS KUSAINIWA KWA MIRADI MIKUBWA MITATU YA UJENZI WA BARABARA

Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli atakuwa Mgeni Rasmi katika hafla hiyo ya kusainiwa kwa mikataba ya ujenzi wa miradi hiyo mitatu mikubwa ambayo utekelezaji wake umekuwa ukisubiriwa kwa hamu.
Miradi itakayohusika ni:
i. Mayamaya – Mela (km 99.35)
ii. Mela- Bonga (km 88.8)
Ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kuanzia Mayamaya hadi Bonga yenye urefu wa kilometa km 188.15 umegawanywa katika sehemu mbili ambazo zitakuwa na mikataba miwili tofauti inayojitegemea. Mikataba hiyo itajumuisha ujenzi wa sehemu ya Mayamaya – Mela (km 99.35) na Mela – Bonga (km 88.8).(P.T)
Kujengwa kwa sehemu hii kati ya
Mayamaya na Bonga katika mikoa ya Dodoma na Manyara kutakamilisha
barabara ya lami inayounganisha miji ya Dodoma na Babati kwa upande wa
mkoa wa Manyara. Sehemu kati ya Dodoma – Mayamaya (km 43.6) ujenzi wake
unaendelea kwa kiwango cha lami na kuanzia Babati hadi Bonga (km 19.2)
tayari imekwishakamilika.
iii. Mangaka – Mtambaswala(km 65.5)
Kipande cha barabara kati ya Mangaka hadi Mtambaswala (km 65.5) mkoani Mtwara ni sehemu ya barabara inayoanzia Masasi hadi Mtambaswala (km 120.6) ambako kuna Daraja la Umoja linaounganisha nchi yetu na Msumbiji. Tayari sehemu ya kati ya Masasi na Mangaka (km 55.1) imekwishajengwa kwa kiwango cha lami na hivyo kusainiwa kwa sehemu hii ya Mangaka hadi Mtambaswala kutaifanya barabara hiyo yote kukamilika kwa kiwango cha lami.
Hafla ya kusaini mikataba hiyo mitatu itafanyikia Protea Court Yard Hotel, Ocean road, Upanga jijini Dar es Salaam kuanzia saa 4:00 asubuhi.
iii. Mangaka – Mtambaswala(km 65.5)
Kipande cha barabara kati ya Mangaka hadi Mtambaswala (km 65.5) mkoani Mtwara ni sehemu ya barabara inayoanzia Masasi hadi Mtambaswala (km 120.6) ambako kuna Daraja la Umoja linaounganisha nchi yetu na Msumbiji. Tayari sehemu ya kati ya Masasi na Mangaka (km 55.1) imekwishajengwa kwa kiwango cha lami na hivyo kusainiwa kwa sehemu hii ya Mangaka hadi Mtambaswala kutaifanya barabara hiyo yote kukamilika kwa kiwango cha lami.
Hafla ya kusaini mikataba hiyo mitatu itafanyikia Protea Court Yard Hotel, Ocean road, Upanga jijini Dar es Salaam kuanzia saa 4:00 asubuhi.
No comments
Post a Comment