Zinazobamba

TATOA WAJIPANGA KUMSHITAKI MAGUFURI, WADAI AMEWASABABISHIA HASARA KUBWA

Pinda amponza Waziri Magufuli


Waziri Mkuu Mizengo Pinda (Kulia) akizungumza jambo wa waziri wa Ujenzi John Pombe Magufuli.Waziri Mkuu amempongeza Magufuli kwa jitihada zake za kuondoa kero barabarani 
Na Hadija Jumanne.Mwananchi
 
 
Kwa ufupi
Chama hicho kimesema hasara hiyo imekuja baada ya kutoa agizo kwa wamiliki wa magari makubwa ya mizigo kutozwa asilimia tano kwa kila gari litakalozidisha uzito na kuagiza kurudiwa kwa utaratibu wa zamani wa msamaha wa asilimia tano ya tozo hiyo.
 
Dar es Salaam. Chama cha Wamiliki wa Malori nchini (Tatoa) kimekusudia kumshtaki mahakamani Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, kwa kuwasababishia hasara wamiliki wa malori nchini.
Pia kimesema Serikali imepoteza zaidi ya Sh30 bilioni kutokana na mgomo wa siku tano.
Chama hicho kimesema hasara hiyo imekuja baada ya kutoa agizo kwa wamiliki wa magari makubwa ya mizigo kutozwa asilimia tano kwa kila gari litakalozidisha uzito na kuagiza kurudiwa kwa utaratibu wa zamani wa msamaha wa asilimia tano ya tozo hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, kwa niaba ya Chama cha Wamiliki wa Malori nchini, Mkurugenzi wa Kampuni ya Usafirishaji ya Simba, Azim Dewji , alisema chama chake sasa kinafanya mahesabu ili kujua hasara ambayo kila kampuni imepata katika kipindi cha mgomo.
Alisema baada ya hatua hiyo, wamiliki wa malori watachukua hatua za kisheria dhidi ya waziri huyo.
Hatua hiyo imekuja siku moja baada ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kufuta agizo lililotolewa na Dk Magufuli la kuwataka wamiliki wa magari makubwa ya mizigo kutozwa asilimia tano kwa kila gari, litakalozidisha uzito.
Dewji alisema sekta ya usafirishaji ni sekta muhimu katika kukuza uchumi kwa kuwa inaajiri watu zaidi ya milioni moja sawa na mara nne ya wapigakura wa Waziri Magufuli hivyo, hakupaswa kutumia ubabe kwenye suala hilo.
Dewji alisema Waziri Magufuli alipaswa kupelekwa kwenye propaganda za chama kwa sababu ndio sehemu inayomfaa kwa ajili ya kupiga propaganda na sio kuwa waziri.

No comments