MAUAJI YA MWINIMSANGA,MKE WA MAREHEMU AMSHUMTU KAMISHINA KOVA KOVA KWA KUUKANA UKWELI
Hivi karibuni kamishina wa polisi kanda maalum ya daresalaam
DCP Suleimani Kova aliitisha mkutano na waandhsi wa habari kuzungumzia mauaji
ya Kijana Suleimani Mwinyimsanga aliuawa
kinyama usiku wa julai 19 huku muuaji halisi akiwa bado hajatambulika
Akizungumza katika mkutano huo kamishina ametangaza kifo cha
Bw. Suleimani lakini akishindwa kuthibishwa kuwa jeshi lake ndilo chanzo
kikubwa cha kifo cha mtu huyo ambaye mwili wake umekutwa na majeraha makubwa ya
kupigwa sehemu zote za mwili wake wakati ukioshwa kiasi cha kufikia baadhi ya
viongo vyake kuvunjwa vunjwa
| KAMISHINA WA POLISI KANDA MAALUM YA DARESAALAAM AKIWA KATIKA MOJA YA MIKUTANO YAKE NA WAANDISHI WA HABARI, KOVA AMESEMA HANA HAKIKA KAMA JESHI LAKE LIMESHIRIKI KATIKA MAUAJI YA KIJANA HUYO |
Kamishina kova, kwa mujibu wa maelezo ya Mtoto wa
marehemu,Jophrey Issa ambaye amekili kuwa
kushuhudia askari wako wakimpiga Bw. Suleimani huku wakimtaka aonyeshe
kitu asichokijua, wakati walipompeleka nyumbani kwake kwa niaba ya kukagua uwepo wa walichotaka kumtuhumu nacho katika
mchana huo wa julai 19 iweje leo hii useme wanajeshi wako hawajaweza kuhusika
na mauaji ya kijana huyo
Lingine kamishina
wangu wa kanda maalum ambayo ama hakika inashughulika na mambo maalum kama
mwenyewe ulivyozoea kusema, baada ya kifo cha Bw. Sulimani pia mmetangaza
kupatikana kwa silaha ambayo ilidhaniwa kuwepo nyumbani kwa Bw. Selemani, je
silaha hiyo ilipatikana mikoni mwa nani na ni kwanini mlichukua hatua ya
kuficha maiti ya Mwinyimsanga kwa muda wa siku tano,mlikuwa mnataka kufanyia
kazi gain hasa?
| MKE
WA MAREHEMU BI HONORATA GIDO AKIWA MWENYE HUZUNI NJE YA OFISI KITUO CHA
SHERIA, MAMA HUYO ALIENDA KUOMBA MSAADA WA KISHERIA MAMA HUYO ANADAI
MUME WAKE AMEULIWA KINYAMA NA JESHI LA POLISI. |
Ama hakika nina maswali mengi sana
ambayo kwa sasa najiuliza kuhusu mauaji ya Mtanzania huyu ambaye hata kama ni kweli mualifu lakini haki ya kutoa uhai wake
wameipata wapi
Ikumbukwe kuwa kwa sasa familia yake inalia na kusaga meno,
mtu wao muhimu ambaye alikuwa anafanya kila liwezekanalo ili watoto wake waweze
kwenda shule tayari ameshaporwa uhai
wake, unadhani nini hasa kitatokea katika familia hiii, hili ni swali pia
ambalo ninajiuliza
Kamishina wangu wa kanda maalum, sasa nimeshudia leo hii
jeshi lako likipelekwa kituo cha haki za binadamu wakishutumu jeshi lako
kushiriki katika mauaji ya Bw. Selemani Mwinyimsanga
Kwa uelewa wangu mdogo hatua hiyo ni mwanzo wa kuchafua
heshima yako iliyojengeka kwa kipindi cha miaka mingi ya utumishi wako ambao
mpaka leo wananchi wa jiji la Daresalaam wamekuwa wakikupigia upatu kuwa
unafanya vizuri sana
katika suala zima la utendaji kazi,
Katika kupeleka malalamiko hayo ya msingi, Mke wa Marehemu
Bi.Honorata Gido amesema wameamua kufikia hatua hiyo baada ya kugundua kuwa
jeshi la polisi halina nia njema na familia hiyo, kwani kwanza kabisa walificha
maiti ya mume wake kwa kipindi cha siku tano katika hospitari ya mwananyamala,
pili wamempiga mume wake kwa kosa ambalo halikuthibishwa mahakamani na tatu
kuondoa uhai wa mtu wamekiuka katiba na sheria ya jeshi la polisi
wanaloliongoza
Naye kwa upande wake Mlezi ambaye ameteuliwa na familia ya Bw.
Selemani Mwinyimsanga kusimamia suala hilo
kwa sasa Bw.Joachim Mgembe amebainisha wazi kuwa jeshi la polisi halina sababu
ya kukataa kuhusika na mauaji ya kijana wao kwani kila dalili na ushahidi upo
wa kuthibitishwa mauaji hayo yalliyofanywa
na polisi
Polisi wapo kwa kulinda wananchi kama
inafikia hatua mtu mmoja anachukua sheria mkononi mwake na kuua bila mtuhumiwa
kuthibishwa mahakamani hapo kuna tatizo na ndio maana tumekuja kitua cha haki
za binadamu kulilia haki ya kijana wetu Bw. Selemani Mwinyimsanga
Kwa upande wake kova amekana kuwa jeshi lake limeshiriki
kwa mauaji ya kijana huyo lakini ameunda tume ya kuchunguza mauaji ya kijana
huyo na watu waliohusika waweze kuchukuliwa hatua mara moja
“sina hakika kama ni kweli
jeshi langu lihusika na mauaji ya Bw. Selemani lakini nanachoweza sema ni
kwamba ninaunda tume kuchunguza suala hilo na kama ikigundulika kuwa askari
amehusika na mauaji hayo atachukuliwa hatua au kama kuna raia yeyote ambaye
amehusika katika mauaji hayo naye atashughulikiw” alisema Kamishina DCP
Suleimani Kova
| JOACHIM MGEMBE AKIWA NA MKE WA MAREHEMU BI. HONORATA GIDO, WAKIPOZI KWA PICHA BAADA YA KUFIKA KATIKA KITUO HICHO, WANANDUGU HAO WAMEFIKA KATIKA KITUO HICHO ILI KULILIA HAKI ZA NDUGU YAO BW. SELEMANI |
| HAPA WAKIWA NJE BAADA YA KUTOA MALALAMIKO YAO |
.
No comments
Post a Comment