Zinazobamba

JUKWAA LASEMA UCHAGUZI ZIMBABWE ULIKUWA WA HAKI,HAUKUWA WA UKATILI KAMA WA 2008

KIONGOZI WA MSAFARA WA JUKWAA LA KATIBA TANZANIABI AISHA ABDULA AKIFAFANUA JAMBO MBELE YA WAANDISHI WA HABARI. ASHA AMESEMA UCHAGUZI ULIKUWA HURU NA HAKIIIIIIIIIIII,KUSHOTO KWAKE NI EBRONI MWAKAGENDA AMBAYE NI MJUMBE WA BARAZA HILO.



JUKWAA la katiba Tanzania limesifu mchakato mzima wa uchaguzi wa nchini  zimbabwe ulivyoendeshwa na kusema kuwa mchakato huo ulikuwa wa utulivu mshikamano na amani katika maeneo yote ya nchi hiyo ikilinganishwa na uchaguzi wa mwaka 2008

Akizungumza na waandihsi wa habari ofisini kwake mwemyekiti wa jukwaa hilo Bw. Deusi Kibamba amesema katika uchaguzi huo ambao wao walialikwa kama waangalizi wa nje waliweza kuangalia katika majimbo yote makubwa ya nchini Zimbabwe na kubaini uwepo wa hali ya utulivu, mshikamano na amani katika maeneo hayo.
Majimbo ambayo waangalizi wa jukwaa la katiba walifanikiwa kuhudhulia na kujionea mchakato wa upigaji kula ni pamoja na majimbo ya Mashonaland (Harare),Matebeleland (Bulawayo) na Manicaland (Mutare) ambako majimbo yote hayo kumeonekana hali ya amani ikitawala

Katika hatua nyingine Bw. Kibamba ametaja baadhi ya kasoro ndogondogo ambazo zimejitokeza katika uchaguzi huo ili Tanzania kama nchi ambayo pia tutafanya uchaguzi mwaka 2015 tuweze kujifunza kutoka kwao na kuchukua hatua stahiki kabla hatujafika siku ya uchaguzi

Miongoni mwa kasoro hizo ni pamoja na kuchapishwa karatasi nyingi za kupigia kura kuliko idadi kamili ya walioandikishwa kupiga kura,hivyo kuongeza dhana ya wizi wa kula kwa vyama vya upinzani


No comments