Zinazobamba

SEMINA JUU YA MATUMIZI YA MITANDAO KUFANYIKA MORO,JUMLA YA WADAU 150 KUSHIRIKI PALE NASHERA HOTELI


Naibu waziri wa mawasilano sayannsi na teknolojia MH. JANUARY MAKAMBA  atafungua semina ya uasalama wa matumiz ya komputa na mitandao yake katika nyanja zote.           
Semina  hiyo imeandaliwa na Taasisi ya ISACA Tanzania kwa kushirikiana na NRD EAST AFRICA  ,semina hiyo ijulikanayo kama Cyber  defense east africa 2013 itawashirikisha watu zaidi ya 150  itafanyika kwa siku tatu kuanzia tarehe 28 mpaka 30 mwezi wa nane katika mji wa morogoro.
Akizungumza na blogu hii rais wa ISACAT TANZANIA ndugu Boniface Francis Kanemba alisema kuwa semina hiyo italenga kwa kina kutoa mafunzo kwa wataalamu wa TECHNOHAMA haswa wale wanaohusika na uasalam a wa mitandao hiyo kutoka pande zote mbalimbali za dunia yakiwemo makampuni  kutoka nchi za ulaya ,amerika na afrika kusini.
Naibu Waziri wa Mawasiliano, Mh. Januari Makamba, akizungumza na William Malecela, pembeni ni mkewe Mheshimiwa, Mrs. Makamba,wakiwa katika moja ya shughuli za kitaifa, Makamba atakuwepo katika semina ya usalama wa mitandao utakaofanyika Agust 29

Kanemba alisema kuwa wataalamu hao wataonyesha kwa vitendo mambo mbalimbali yanayofanyika wakati wa kufanya wizi wa mitandao na washiriki wa semina hiyo watashiriki kwa vitendo hivyo ambavyo vimelenga kutoa ufahamu zaidi juu ya kile kinachotokea kwenye mtandao haswa kwa matumizi mabaya kama wizi
Vilevile kila mshiriki atajionea kwa macho yake jin si wizi wa mtandao unavyoandaliwa na kufanyika katika maeneo mbalimbali yakiwemo katika mabenki,serikali ,makampuni ya simu na mengineyo na hivyo kuongeza ufahamu wa jinsi ya kudhibiti uhalifu.
“mafunzo haya ni kwa ajili ya wadau mbalimbali kutoka sekta zote za umma na binafsi pia kutoka nchi zote tano za afrika mashariki yaani tanzaia,kenya,uganda ,rwanda na burundi ,hii ni kutokana na nchi hizi kuwa na changamoto sawa la ongezeko la wizi wa mtandao na matumizi mabaya ya mitandao katika miaka ya hivi karibuni” alisema ndugu Kanemba
Aidha kanemba alisema kuwa tafiti iliyofanywa na kampuni ya Deloitte mwaka 2012 inaonyesha kuwa mabenki ya biahsra kwenye inchi za afrika mashariki yanapoteza takribani zaidi ya shilingi bilioni 80 kutokana na wizi wa mitandao kwa mwaka kiasi ambacho bado kinasadikiwa kuwa kinaweza kuwa zaidi ya ikizingatia juwa matukio mengi huwa hayaripotiwi hivyo kutokuwa na idadi kamili ya fedha zote.
.

No comments