WIZARA YA NISHATI YAANZA KUTOA HUDUMA MAONESHO YA SABASABA

WIizara ya Nishati pamoja na taasisi zake zimeanza kutoa huduma kwa wananchi wanaoshiriki Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba).
Maonesho hayo yameanza tarehe 28 Juni 2026 na yatahitimishwa 13 Julai 2026 katika Viwanja vya Mwl.Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Katika banda la Nishati wananchi wanapata taarifa za miradi na huduma mbalimbali zinazosimamiwa na Wizara.
Aidha, Wizara ya Nishati inatumia maonesho ya SabaSaba kama jukwaa muhimu la kutoa elimu kuhusu nishati safi ya kupikia, umeme na fursa za uwekezaji zilizopo katika Sekta ya Nishati.
Taasisi zilizo chini ya Wizara zinazoshiriki maonesho ya SabaSaba ni Shirika la Umeme Tanzania ( TANESCO) na kampuni zake tanzu, Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania ( TPDC) na kampuni zake tanzu, Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) na Wakala wa Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja (PBPA).
No comments
Post a Comment