Zinazobamba

Mbeto :Jusa hana mbavu za kushindaa na CCM Zbar


Na Mwandishi  Maalum, Zanzibar

Chama Cha Mapinduzi  ( CCM) kimemtaka Makamu Mwenyekiti  wa ACT  Wazalendo , Ismail Jussa Ladhu ,  kushughulika na matatizo yaliomo ndani ya chama chake kwakuwa CCM hana ubavu wa kushindana nacho.

Vile vile  CCM kimemtaka ajue  mambo ya ngowe  huachiwa ngoswe  wenyewe hivyo  asipoteze nguvu zake kukizungumzia CCM. 

Hayo yameelezwa na Katibu  wa Kamati  Maalum  ya NEC  Zanzibar,  Idara  ya Itikadi  , Uenezi na Mafunzo, Khamis  Mbeto  Khamis,  aliyemtaka Jussa akisubiri  kimbunga kitakachokipeperusha ACT oktoba  mwaka huu.

Mbeto alisema Jussa  hajui yalioko serikalini  wala  hafahamu takwimu na data za  wanachama hai  au wapiga kura ambao watakipatia ushindi  CCM    .

Alisema anamtambua vizuri  Jussa  kama ni  kasuku wa kisiasa  ambaye  sauti na uso wake hauna staha wala aibu  ,ndio maana huthubutu hata kubeza  maendeleo  yanayoonekana Zanzibar kwa  wakati huu.

"Mwambieni Jussa apuunguze usanii na porojo  kwenye   majukwaa ya siasa ameschokwa na Wananchi  .Siasa za kibaguzi dhidi ya wazanzibari zimegonga ukuta. Anaowataka waamini  kama hakuna maendeleo wanamsikiliza , wakimcheka na kumpuuza "Alisema Mbeto

Aidha alimtaka Makamu  Mwenyekiti  huyo iwapo ana ushahidi  wa kutosha dhidi ya smz  ikihusika na ubadhirifu  wa mamilioni ya fedha  za umma ,ruksa  afungue mashikata mahakamani.

"Oktoba mwakaka huu panapo uhai na uzima  itafika . Mpira utawekwa katikati ya kiwanja . Mwamuzi atapuliza kipyenga . Mchezo  utachezwa na wananchi  wataamua ipi mbivu na  mbichi" Alieleza Mbeto.

Pia Katibu  huyo Mwenezi  ,alisema hata kama  Jussa ataendelea kulitumia jina la Hayati Maalim Seif Sharif Hamad ,akidhani ACT kitapata mtaji wa kuungwa mkono, hakiwezi kushinda mwezi  oktoba.

Hata hivyo Mbeto alimuasa Jussa na kumtaka aache siasa za ubaguzi kwani  Zanzibar kama  kungekuwa na siasa za kubaguana kwa asili na nasaba  ,yeye ndiye aliyestahili kubaguliwa kuliko mtu yeyote.

"CCM  , Zanzibar na Tanzania  zimekataa siasa za ubaguzi wa aina yoyote  . Tulipinga siasa aina ya siasa  hizo kila mahali  duniani. Jussa huna  uwezo wa kumbagua yeyote Zanzibar   kabla  wewe hajabaguliwa" Alieleza .

Mbeto alimueleza Jussa maamuzi ya CCM yatabaki  kuwa  ya CCM kwani hata ACT  Wazalendo  kilianza kutangaza jina la Othman  .

Masoud  Othman kama ndiye mgombea urais  miaka mitatu iliopita.

"Miaka mitatu iliopita Jussa na wenzake ndani ya ACT   walimtangaza Othman atawania urais  mwaka 2025 Zanzibar . Alipata wapi idhidi ya kutamka hivyo bila azimio la  mkutano Mkuu wa  Taifa  wa ACT? "Alihoji Mbeto

Hakuna maoni