Zinazobamba

CCM:Jussa ni Ian Smith wa Zanzibar


Na Mwansishi Wetu, Zanzibar 

Chama Cha Mapinduzi(CCM)  kimesema Makamu Mwenyekiti  wa ACT  Wazalendo, Ismail  Jussa Ladhu,  kifikra na kiitikadi ni sawa na aliyekuwa kiongozi wa kibaraka Ian Smith mpambe wa sera za  Wakoloni huko South  Rhodesia (Zimbabwe)

CCM kimemtaja ni kibaraka   mkongwe kutokana na ushamba wa  kubeza maendeleo  yanayoletwa na viongozi wa Afrika akishabikia ukoloni.

Hayo yametamkwa na Katibu  wa Kamati  Maalum  ya NEC  Idara ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo , Mbeto Khamis  Mbeto, aliyemwita Jussa ni  kibaraka kama alivyokuwa   smithi au Mtawala wa zamani wa Zaire, Mobutu  Seseseko. 

Mobutu na  Smith walikuwa viongozi wasaliti dhidi ya maendeleo ya Afrika na kuwa mashabiki wakubwa wa sera na misimamo ya kikoloni.

Mbeto  alisema  Jussa amekuwa  mstari  wa mbele kuponda juhudi za SMZ chini ya Rais  Hussein  Ali Mwinyi za  ujenzi  wa shule  za ghorofa,  bila aibu hudai majengo  hayo hayana maana  kwa maendeleo  ya Zanzibar. 

Mara kadhaa Jussa amekuwa akijinasibu yeye  amesoma kwenye maghorofa machache yalioojengwa na utawala wa kifalme.

Alisema Jussa alipaswa kusifu baada ya  kuona watoto wa Wakulima na Wakwezi, sasa  wakisoma  shule zilizo  bora, kinyume chake,  amekuwa  akidai majengo hayo si chochote  kwa maendeleo  ya Zanzibari. 

"Jussa ni  kibaraka mpya miongoni mwa vibaraka wachache waliobaki  Afrika. Ni Ian Smith mpya na kikwazo kwa maendeleo ya Zanzibar pia  akifanana kifkra na Rais  wa  zamani huko Zaire  Mobutu Seseseko  " Alisema Mbeto 

Aidha  Katibu huyo Mwenezi  alisema kinadharia na kiuhalisia , Makamu  huyo  Mwenyekiti  ACT  Wazalendo ,bado anatamani sera za  ukandamizaji chini ya  ukoloni  uliowanyima elimu watoto  wa kiafrika. 

' Jussa  acha kujivunia  shule chache za ghorofa zilizoachwa na Wakoloni .Ni aibu kwako na kwa ACT  Wazalendo .Matamshi yako yanazidi kukinyima kura ACT  kutokana na ulimi  wako  kuwa mchafu " Alisisitiza 

Mbeto  alisema  wakati  Jussa akijigamba  kuwepo kwa shule chache   za ghorofa ndani ya Mji Mkongwe, huko   Kisiwapanza,Fundo, Muwambe , Makunduchi, Paje , Donge na Mtambwe , wakoloni toka Mwaka 1804 hadi 1964 , hawakujenga shule  za ghorofa.

'Mazuri yanayofanyika sasa  ni baada ya Mapinduzi  Matukufu Mwaka 1964.

Watoto  wa  kina Pandu, Jecha, Makame na Simai  wanapata elimu  bora . Hivi sasa huko Kojani  Tumbatu, Kisiwapanza na Kiwani  watoto wa Wakulima na Wavuvi  wanasoma katika shule za  ghorofa za SMZ " Alisema

Hakuna maoni