Zinazobamba

Mtaalam Veta ashauri masomo ya ujuzi yapewe kipaumbele

 




Na Mwandishi wetu

Meneja mahusiano wa mamlaka ya elimu na mafunzo ya Ufundi stadi (VETA), Mh. Sitta Petter amewashauri wazazi/walezi na wanafunzi wa kidato cha nne kwa ujumla wake kuanza kufikilia kusoma mafunzo ya ufundi ili kujipatia ujuzi wakati huu ambao wanasubiri matokeo ya kidato cha tano kutoka

Sitta ametoa rai hiyo Novemba 3, 2023 wakati akizungumza na mtandao wa fullhabariblog katika uwanja wa mnazi mmoja ambako kulifanyika maonesho ya miaka 50 ya Necta.

“Tuna vijana wengi ambao wamemaliza kidato cha nne ambao wanasubiri matokeo kutoka, tunaamini wapo ambao watakwenda kidato cha tano lakini pia wapo watakaokwenda vyuo vya ufundi, tunawaambia wakati huu ambao wapo kipindi cha mpito watumie fursa hii kusoma kozi fupi za ufundi stadi,” alisema

Amesema badala ya kuwapeleka watoto kusoma masomo kwa ajili ya kidato cha tano (Pre-form five), basi watumie muda huo kujifunza ujuzi, kwani mitaala ya sasa inasukuma Zaidi ufundi

Amesema faida ya kusoma ufundi stadi ni pamoja na kuwa katika nafasi nzuri ya kupata ujuzi ambao utakusaidia katika Maisha yako, kwamba kijana ambaye anao ujuzi anakuwa tofauti na yule ambaye bado hana ujuzi.

Mimi niko form five lakini tayari fundi umeme, au fundi magari, inawezekana kabisa hata wakati wa likizo akirudi anaweza kuendeleza fani yake, jambo hili linawezekana kabisa,” alifafanua

Mtoto anapokwenda kusoma Pre-form five halafu hakubahatika kufaulu maana yake mzazi amekula hasara, lakini mtoto naye amepoteza muda wake, lakini akipata ujuzi atakuwa msaada katika familia,” aliongeza

Mtaalam huyo wa masuala ya mahusiano ya umma amesisitiza kusema elimu ya sasa ina mikondo miwili, upo ule wa kawaida lakini pia upo wa mafunzo ya amali, ni vizuri wazazi wakalifahamu hilo na kuandaa Watoto watakaoingia katika makundi hayo

 


Hakuna maoni