RAIS MAGUFULI MGENI RASMI SIKU YA SHERIA NCHINI,SOMA HAPO KUJUA
![]() |
Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Prof. Ibrahim Hamis Juma
akiongea na wanahabari (hawapo pichani) kuhusu Kilele cha Maadhimisho ya Siku
ya Sheria nchini kitakachofanyika hivi karibuni katika viwanja vya Mahakama
vilivyopo jijini Dar es Salaam.
|
Rais John Pombe Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni
rasmi katika kilele cha maadhimisho ya siku ya Sheria nchini zitakazofanyika
mwanzoni mwa mwezi ujao katika viwanja vya Mahakama jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam Kaimu
Jaji Mkuu Prof. Ibrahim Hamis Juma amesema mahakama itawaelimisha wananchi
jitihada mbalimbali ilizochukua zenye lengo la kuboresha huduma zake kupitia
mpango mkakati wa miaka mitano inaoutekeleza katika kutoa haki kwa wakati na
kuwezesha ukuaji wa uchumi.
Amesema kabla ya kilele cha maadhimisho hayo,
mahakama itafanya matembezi maalum yatakayoongozwa na Rais Mstaafu Mh. Ali
Hassan Mwinyi na yataanzia Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kuishia
katika viwanja vya Mnazi mmoja.
Katika matembezi hayo Mhe. Rais Mstaafu Mwinyi
atazindua rasmi maadhimisho ya wiki ya elimu ya sheria ikiwa ni sehemu ya
sherehe za kuelekea maadhimisho ya kilele cha siku ya sheria nchini.
Aidha ametoa rai kwa wananchi kutembelea sehemu zote
zilizoandaliwa kwa ajili ya utoaji elimu ya sheria nchini kwa ajili ya
kujifunza na kupata huduma mbalimbali za Kisheria.
Alizitaja huduma hizo ni pamoja na taratibu za
ufunguaji mashauri katika ngazi mbalimbali za mahakama, taratibu za kesi za
mirathi, taratibu za kesi za dhamana, taratibu za rufaa, ndoa na talaka,
taratibu za kupokea na kushughulikia malalamiko na Msaada wa Kisheria
![]() |
Jaji
Kiongozi wa Mahakam Kuu Tanzania Jaji Ferdinandi Wambali (kushoto) akiongea na
wanahabari (hawapo pichani) kuhusu Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Sheria
nchini kitakachofanyika hivi karibuni katika viwanja vya Mahakama vilivyopo
jijini Dar es Salaam.
|
Maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini hufanyika kila
mwaka mwanzoni mwa mwezi wa pili na mwaka huu yamebeba ujumbe wa Umuhimu wa
Utoaji Haki kwa Wakati Kuwezesha Ukuaji wa Uchumi.
![]() |
Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Katrina Revocati akiongea na
wanahabari (hawapo pichani) kuhusu Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya
Sheria nchini kitakachofanyika hivi karibuni katika viwanja vya Mahakama
vilivyopo jijini Dar es Salaam
Post Comment