RAIS MAGUFULI AVUNJA UKIMYA WA KUSAFIRI NJE,AANZA RASMI KUSAFIRI,SOMA HAPO KUJUA
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, tarehe 28
Januari, 2017 ameondoka nchini na kuelekea Mjini Addis Ababa nchini
Ethiopia ambako atahudhuria mkutano kilele wa 28 wa wakuu wa nchi
wanachama wa Jumuiya ya Umoja wa Afrika (AU) unaoendelea nchini humo.
Katika
uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam,
Rais Magufuli ameagwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri
Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa na Viongozi wa Mkoa wa Dar es Salaam
wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa Bw. Paul Makonda.
Pamoja
na kuhudhuria Mkutano huo, akiwa Addis Ababa Rais Magufuli anatarajiwa
kukutana na kufanya mazungumzo na viongozi mbalimbali wa Bara la Afrika
wanaohudhuria Mkutano huo.
Hii
ni ziara ya kwanza ya Mhe. Rais Magufuli nje ya Afrika Mashariki tangu
aingie madaraka kuongoza Serikali ya Awamu ya Tano ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania tarehe 05 Novemba, 2015
Jaffar Haniu
Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
A
Post Comment