BENKI YA DCB YAZIDI KUWAJALI WATEJA WAKE,YAJIPANGA KUFANYA HIVI KWA MWAKA HUU,SOMA HAPO KUJUA
Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya DCB,Edmund Mkwawa |
NA KAROLI VINSENT
Imeelezwa
kuwa moja ya kipaumbele cha benki ya DCB kwa mwaka huu nikutoa huduma ya mikopo
kwa vikundi kwakuwa ndio chimbuko kuu la kuanzishwa kwake.
Hayo yameelezwa na Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo Edmund Mkwawa mwishoni mwa wiki wakati wa hafla ya utaoji zawadi kwa tawi la Magomeni ambalo ndio
mshindi wa huduma za Vikundi kwa wateja wake, ambapo amesema kuwa huduma hiyo imelenga zaidi kuwa hudumia wajasiriamali wadogo ili kuinua Maisha yao.
"Kama mnavyojua huduma hii ni chimbuko kuu la kuanzishwa kwa DCB ikilenga zaidi kuwahudumia wajasiriamali wadogo ambao walikuwa hawapati huduma za kifedha kwenye mabenki makubwa ili kuinua hali ya Maisha yao". Alisema Mkwawa
Mkwawa amewapongeza washindi na kuwakumbusha kuwa mafanikio yoyote yanatokana na uongozi imara na kuwataka wengine kuiga mfano na kujituma maradufu ili kuongeza mafanikio ya taasisi hasa katika kipindi hiki ambapo biashara imekuwa ngumu.