Zinazobamba

HOSPITALI YA AGAKHAN YAWAJALI WATANZANIA,SASA WAJA NA KITU MUHIMU,SOMA HAPO KUJUA



 agakhan-2
Wanawake na watoto nchini waliopata majeraha ama makovu kwenye miili yao hospitali ya Agakhan ili waweze kufanyiwa upasuaji wa kurekebisha viungo vyao viweze kuwa katika hali ya awali.

yaliyosababishwa na manyanyaso ya kijinsia, ajali na moto wametakiwa kuhudhuria

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam mwakilishi kutoka wizara ya afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Dk. Ally Sadiki amesema kuwa upasuaji huo utafanywa kwa ushirikiano wa hospitali ya taifa ya muhimbili ambapo maatibabu ya kurekebisha viungo ya tadumu kwa kipindi cha miaka miwili.

Amebainisha kuwa kuwepo kwa huduma hiyo ni moja ya mikakati ya Serikali ya kuhakikisha inahudumia wananchi wake hasa wale wasiokuwa na uwezo wa kumudu gharama za matibabu na kuongeza kuwa ni vizuri wananchi wakashiriki kupata huduma hiyo.
Naye muuguzi kiongozi idara ya upasuaji kutoka katika hospitali ya Agakhan Zainabu Mallya ameeleza kuwa huduma hiyo inatolewa mahususi kwa watoto na wanawake kwa kuwa wao ndiyo kundi kubwa la watu wanaopata ulemavu wa viungo kutokana na manyanyaso ya kijinsia na matibabu yote yatatolewa bure bila gharama.