Zinazobamba

Tume ya Mufti yakabidhi Ripoti ya Uchunguzi wa Mali za BAKWATA Dar

dsc_1123
Tume iliyoundwa na Mufti wa Tanzania , Sheikh Abubakar Zubeir mapema leo Novemba 24 imekabidhi “Ripoti ya Tume ya Mufti” ya Mali za BAKWATA  kwa mkoa wa Dar es Salaam   mbele ya wanahabari  na kueleza kuwa mambo yote wameyaorodhesha humo na baada ya kuipitia Mufti mwenyewe ndiye mwenye mamlaka ya kuweka wazi.
Akipokea Ripoti hiyo, Mufti amebainisha kuwa,  kazi iliyofanywa ni nusu ya kazi yenyewe iliyotarajiwa kuipata na kwa unyeti wa jambo hilo ameamua kuwaongezea muda wa siku 90, yaani miezi mitatu ili waweze kuzunguka nchi nzima.
“Nashukuru kwa kazi muliyofanya. Kwa unyeti wa jambo lenyewe nimeamua kuwaongezea muda kwani BAKWATA ipo karibu nchi nzima na nawongezea miezi mitatu. Kwa kuwa sijui kipo ndani ya ripoti hii mpaka noisome, nadhani baada ya hapo nikisha ipitia nitayafanyia kazi” ameeleza Mufti , Sheikh Zubeir.
Tume hiyo  yenye  jopo la Wajumbe Nane akiwemo Mwenyekiti wa Tume hiyo Sheikh Abubakar Khalid na akisaidiwa na Kaimu Mwenyekiti wa tume Sheikh Issa Othuman Issa  na wajumbe wengine sita akiwemo Katibu wa tume, Mwalimu Salim Ahmed Abeid na wengine wanne.


dsc_1100
Sheikh Abubakar Khalid akimkabidhi Mufti wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir ripoti ya Tume ya Mufti iliyochunguza Mali za BAKWATA  kwa mkoa wa Dar es Salaam. Kushoto ni Kaimu Mwenyekiti wa tume hiyo, Sheikh Issa Othuman Issa.
dsc_1117
Sheikh Abubakar Khalid akimkabidhi Mufti wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir ripoti ya Tume hiyo.Kushoto ni Kaimu Mwenyekiti wa tume hiyo, Sheikh Issa Othuman Issa.
Mufti wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir  
dsc_1135
Kaimu Mwenyekiti wa tume ya Mufti, Sheikh Issa Othuman Issa akielezea namna Tume ilivyofanya kazi yake na kukabidhi ripoti hiyo mapema leo
dsc_1138
Mwenuyekiti wa Tume ya Mufti, Sheikh Abubakar Khalid
dsc_1144
Baadhi ya wajumbe wa tume hiyo
dsc_1174
Ripoti ya tume hiyo
Makabidhiano ya ripoti hiyo
dsc_1160
Mufti wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir  (katikati) akiwa pamoja na jopo la tume hiyo muda mfupi baada ya kukabidhiwa ripoti.
PICHA ZOTE NA ANDREW CHALE