SIRI YAFICHUKA YA SERIKALI KUMPORA SHAMBA SUMAYE,KUMBE YALIYOMKUTA MBOWE, LOWASSA NA KUBENEA YATAJAWA KWA SUMAYE,SOMA HAPO KUJUA
NA KAROLI VINSENT
WAKATI Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Joh
Magufuli ikiwa ni kama imezamilia kuwakomoa vigogo wa Upinzani,baada ya serikali hiyo ikiwa teyari imeshamfukuza kwenye nyumba ya shirika la Nyumba la Taifa
(NHC) mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema,Freeman Mbowe kwa
kile inachokidai mwenyekiti huyo
ameshindwa kulipa kodi ya pango katika jengo.
Na baadae serikali hiyo inayojiita
"serikali ya Hapa kazi” pia ikawa pia imekifungia kituo cha Redio Five cha Arusha ambacho
kinamilikiwa na Waziri mkuu wa Zamani
ambaye alikuwa mgombea wa Urais wa Chadema kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka
jana,Edward lowassa kwa kile inachosema serikali hiyo kuwa kituo hicho kimerusha taarifa za
uchochezi.
Mbali na Lowassa,serikali hiyo ikiwa imeyafungia Magazeti ya Mawio,Mseto ambayo yanamilikiwa na Mbunge wa jimbo la Ubungo (CHADEMA),Saed Kubenea kwa hoja ya magazeti hayo yanaandika habari za uchochezi.
Sasa ni kama zahama
kama hayo ya hapo juu. yamemkuta pia Waziri mkuu Mstaafu wa awamu ya
tatu,Fredrick Sumaye ambaye alikuwa ni mmoja wa wasemaji
tegemeo katika mikutano ya kampeni ya Uchaguzi Mkuu uliopita ya Umoja wa Katiba
ya Wananchi (Ukawa).
Baada ya Rais Magufuli
kumnyang’anya shamba lake lenye ukubwa wa hekta 33
kwa kile kilichoelezwa kushindwa kuliendeleza.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally
Hapi amesema kuwa Serikali imefikia uamuzi huo baada ya Sumaye kushindwa
kuliendeleza kama notisi ya siku 90 ilivyoeleza.
“Oktoba 28, mwaka huu. Rais John
Magufuli alibatilisha hati ya kumiliki ardhi ya shamba namba 3074 lililopo
Mabwepande. Shamba hili lilikuwa na hati namba 53086. Jina la mmiliki
lililoandikwa katika hati ni Frankline Sumaye,” amesema Hapi.
Akizungumzia hali hiyo Kigogo kutoka
ndani ya serikali Aliyejiiita kuwa anamapenzi mema na upinzani wa nchi hii huku pia hakutaka jina lake litajwe mtandaoni aliumbia mtandao
wa ‘Fullhabari.blogs” hatua hiyo
inalengo la kumnyamazisha Waziri mkuu huyo ambaye anaushawishi mkubwa nchini na
ambaye anatajwa uwenda ni mtu hatari kwenye uchaguzi wa Mwaka 2020.
“Tatizo jeraha la uchaguzi wa mwaka
jana linawatesa viongozi wa nchi hii,hivi hoja la sumaye kutoliendeleza shamba
ziko wazi ni kwamba kuna kesi mahakamani,sema viongozi hawa wanauoga na sumaye
kuelekea uchaguzi wa mwaka 2020,wanajua sahav hali ya nchi mbaya hakuna ajira mpya,wanafunzi hawa mikopo,uchumi upo vibaya,mabenk yanafirisika,umasikini umeongezeka”:
“Kwani kuna vigogo wangapi ndani ya
Chama cha Mapinduzi CCM,wanamashamba na wameshindwa kuyaendeleza,leo wanamuona
Sumaye tu,nakwambia hawa watawala wanauoga ndugu,"kimesema Chanzo chetu hicho.