Zinazobamba

SHIRIKA LA NDUGE LA ATCL LAENDELEA KUFAGIA WAFANYAKAZI,YAWAONDOA WAKURUGENZI WAKE,SOMA HAPO KUJUA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhKvxGOy7ozn1qxBJtZdjeHe5mdk7QqnbNn-9oPKK66H6G7Bd8ggWzP3yqVgDHuurUqSRdc4bB88Pd1HkeHOVQrw-bQj-q3zKlLZ2bPW2a9QG85Af8fIGxTTfOYIlg4uAsIXCxhdZYmSgjt/s1600/WhatsApp+Image+2016-11-25+at+12.59.20.jpeg
 Mwenyekiti wa Bodi ya ATCL,Mhandisi Emmanuel Korosso(katikati) akizungumza na Waandishi wa Habari leo katika Ofisi za Shirika hilo,Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika,Ladislaus Matindi,kulia ni Mjumbe wa Bodi,Dkt. Mussa Mgwata
BODI ya shirika la ndege nchini(ATCL) imeagiza kuondolewa  baadhi  ya mameneja katika nafasi zao ndani ya shirika hilo  baada ya kubainika wanautendaji dhaifu pamoja na kuwepo na viwango  vidogo vya elimu visivyokidhi katika nafasi hizo.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.

Hata hivyo,Bodi hiyo imetangaza kuzindoa  idara tano za ukurugenzi ndani ya shirika hilo baada kubainika pia hazina tija,
Idara hizo ni kurugenzi ya  idara ya Biashara,Kurugenzi ya dara ya Ufundi,kurugenzi ya idara ya oparesheni,kurugenzi ya idara usalama pamoja na kurugenzi ya idara ya fedha.
Huku pia Bodi hiyo ikitoa maelekezo kwa wakurugenzi wote waliokuwa wamekaimu katika idara hizo ambazo zimeondolewa  wametakiwa kurudishwa katika nafasi za chini  ambazo sio Menejimenti

Akitangaza maazimio hayo ,leo Jijini Dar es Salaam,Mwenyeti wa Bodi ya (ATCL),Mhandisi Emmanuel Korosso amesema mara baada ya shirika hilo kupokea ndege mpya aina ya Bomardier Q400,na kuanza safari zake sehemu mbali ndani ya nchi na nje ndipo wakaitisha kikao cha Bodi ya wakurugenzi ya shirika hilo kwa lengo la kufanya uamuzi wa kimuundo wa kuboresha shirika hilo.
Amesema Wameibaini kuwepo kwa wakurugenzi ndani ya shirika hilo ambao ni wadhaifu pamoja kutokizi kielimu.
“Katika kiko chetu cha Novemba 18,tumebaini watendaji hawa wanauwezo mdogo  wa elimu ambao mtu hawezi kuwa na elimu ndogo kiasi kile hakawa mkurugenzi,tena mbali na elimu ni wadhaifu mnao kiutendaji kabisa na hatuwezi tukawa nao kwenye shirika hili”,amesema, Mhandisi Korosso.
Mhandisi Korosso amesema Bodi yake imuagiza Mtendaji mkuu wa (ATCL) Mhandisi  Ladislaus Matindi kuwaondoa wakuregenzi wanaokaimu nafasi zao na kupangiwa katika nafasi za chini  ambazo sio menejimenti au kupangiwa katika vituo vya  Mikoani.
Aidha,Bodi hiyo  katika kikao chake hicho ,ilipitisha mpango wa biashara wa muda (Interim Business Plan) na Muundo wa muda (Interim organization Structure)ili kukizi matakwa ya sasa ya ATCL kutokana na malengo iliyojiwekea katika kipindi cha miaka mine.
Mbali na hayo Bodi hiyo imemuagiza Mtendaji wa shirika hilo kutangaza nafasi zozote ambazo anaona kuwa kuna umuhimu wa kuajiri watu wengine ili kuongeza kasi za ufanyaji kazi katika shirika hilo.

Mhandisi Korroso ameuagiza pia Mtendaji huyo kutengaza  mara moja