Zinazobamba

Serikali yawashauri Benbros motors ,Yutong Zhengzhou kufungua kiwanda cha magari Tanzania


Waziri wa habari,utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye akishikana mikono na Mkurugenzi Mtendaji wa Benbros Motors Ltd Bw. Noufal Mohammed Es-Haq huku wakielekea katika uzinduzi wa gari jipya aina ya F12 .Wanaoangalia kwa karibu kutoka kushoto ni Mwakilishi kutoka ofisi ya makamishna mkoa wa Pwani Bw. Shangwe Tamal na kulia ni Bw. M.A. Es-Haq.

Waziri wa habari, utamaduni, sanaa na michezo, Bw. Moses Nnauye akifurahia jambo mbele ya Wateja wa Kampuni ya Benbros. Aliyechuchumaa ni Injinia ufundi wa Kampuni hiyo Bw. Frank Lee




Kampuni za Benbros Motors Ltd na Yutong Zhengzhou zimeshauriwa kuanzisha
 kiwanda cha magari hapa Nchini kusudimabasi yao yaweze kutengenezwa 
na kusambazwa hapahapa nchini.
 
Akizungumza katika sherehe za uzinduzi wa gari jipya aina ya F12 kutoka kampuni 
ya usambazaji ya Benbros Motors Ltd, Waziri wa habari, utamaduni,
 Sanaa na michezo Mh. Nape Nnauye amesema Serikali ipo tayari kutoa 
ushirikiano wowote ili kufanikisha zoezi hilo.
 
Amesema, shauku kubwa ya Serikali ni kuona magari aina ya
 Yutong sasa yanatengenezwa hapa nchini na kuachana kabisa
 na zoezi la kuagiza vifaa kutoka nje ya nchi.
Aidha akizungumzia uzinduzi wa gari jipya aina ya F12 
linalotarajiwa kuingizwa sokoni hivi punde, Waziri Nnauye
 amekili kuwa gari hilo limekidhi ubora kufuatia kuwa na vitu vyote
 muhimu vinavyotakiwa kwa mujibu wa sheria.
 
Alisema ‘ nimefurahishwa na naomba niwapongeze Benbros Motors
 Ltd na Yutong Zhengzhou juu ya uzinduzi wa basi mpya aina
 ya  F12 Plus, kwani  bus hili lina sifa zote kwa barabara zetu na
 usalama wa raia.
Amesema sifa za basi hilo jipya, linaitofautisha na mabasi mengine 
barabarani na kulifanya liwe mfalme,kwani naambiwa lina uwezo 
mkubwa wa kubeba mizigo jambo ambalo linapendwa na abiria
 wengi.
 
Katika hatua Nyingine meneja mauzo wa Benbros Motors Ltd Bw. Albert Currusa amesema kampuni yake kwa kushirikiana na kampuni ya Yutong wamejipanga kuendelea kutoa huduma bora kwa Watanzania.

Amesema Basi mpya Aina ya F12 plus inayozinduliwa ni basi yenye sifa ya kipekee kutoka kampuni ya Yutong ambayo anahakika wateja wataifurahia ikishaingia sokoni.
Akitaja sifa za basi hilo, Albet amesema Basi hilo ina uwezo mkubwa wa kubeba mzigo yenye uzito mkubwa, ikiifanya kuwa mfalme barabarani kwa usafiri ya abiria.
Pia basi hilo linakuja na video za kisasa ambayo inaitwa (Videoon demand) na ina WifI pia.  
Ameongeza Hata kama Wifi haipatikani bado una uwezo wa kuangalia video, kusiliza radio, kucheza michezo bure upo Kwahiyo, safari yako itakuwa nzuri tu.
Siti zake zimetengezwa kwa ngozi kusudi abiria wawe na raha wakati wako ndani ya basi hilo. Screen ya TV iko kwenye sehemu ambapo abiria anakuwa yuko comfortable. Pia kuna screen zigine kwa abiria ambao wanakuwa wamekaa nyuma ya basi. Pia kuna port za USB kusudi abiria aweze kupata burudani ya kutosha.