Zinazobamba

TCRA YAIFUNGULIA MAGIC FM REDIO .PIA YAENDELEA KUING'ANG'ANIA REDIO YA LOWASSA,SOMA HAPO KUJUA

Seebait.com 2016

Pichani ni Meneja mipango wa Kituo cha Redio Magic Fm orest Kawau ambaye ni  miongoni mwa watangazaji wa kipindi cha Morning Magic picha na Maktaba



KAMATI ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasilioni nchini (TCRA) Imekifungulia Kituo cha Redio  cha Magic Fm cha DaresSalaam  na kuhiruhusu kuendelea na matangazo yake pamoja na kuiipa onyo kali.

Hata Hivyo,Kamati hiyo imekifungia kwa miezi mitatu pamoja na kuitoza faini ya milioni 5 kituo cha Redio Five cha Mkoani Arusha kituo hicho ambacho kinamilikiwa na Waziri Mkuu wa Zamani,Edward Lowassa.

 Akitoa hukumu hiyo leo Jijini dare s Salaam,Mwenyekiti wa Kamati hiyo,Joseph Mapunda amesema Mamlaka hiyo imetoa hukumu hiyo baada ya kujilidhisha pande zote mbili.


Mapunda, amesemakuwa kituo Redio Five  kilirusha maneno yaliyo tamkwa na Lema ambayo yalikuwa yakihamasisha wananchi kushiriki katika maandamano ya Ukuta yaliyopigwa marufuku na Jeshi la Polisi.

“Maneno ya Lema yalilenga kuhaasisha wananchi kupambana na jeshi la polisi na hivyo kusababisha uvunjif
u wa amani na kuhatarisha usalama wa Taifa,” amesema.
Mapunda amesema uamuzi huo umetolewa na kamati hiyo baada ya kamati hiyo kusikiliza maelezo ya utetezi yaliyotolewa na wa Uongozi wa Redio 5 Arusha.
“Baada ya kusikiliza maelezo ya utetezi kamati imeridhia kuwa kipindi cha matukio kilikiuka baadhi ya kanuni za maudhui namba 5(a,b,c,d,f,h) 6(2) (b, c) na 18 (1) (b),” amesema.
Ameongeza kuwa ” kituo hicho kinatozwa faini ya sh. Milioni 5 ambazo zitatakiwa kulipwa ndani ya siku 30 kuanzia leo, kinafungiwa kwa miezi 3 na kuwekwa chini ya uangalizi maalumu kwa muda wa Mwaka 1 baada ya kipindi cha kufungiwa kumalizika, “
Hata hivyo, Mapunda amesema haki ya wahusika kukata rufaa dhidi ya uamuzi huo iko wazi ndani ya siku 30 kuanzia leo.
Kwa upande wa kituo cha redio cha Magic Fm ambacho nacho pia kwa mujibu wa kamati hiyo kinadaiwa kukiuka kanuni za maudhui kupitia kipindi chake cha Morning Magic kipengele cha Paka Rangi ambapo kilirusha maneno yanayodaiwa kumkejeli rais na wananchi, kimepewa onyo kali pamoja na kutakiwa kuomba radhi kwa muda wa siku tatu mfululizo.
“Baada ya kusikiliza na kutafakari kwa kina maelezo ya utetezi yaliyotolewa na Uongozi wa Magic Fm Redio, Kamati ya Maudhui imeridhika kuwa kipindi cha Morning Magic kilikiuka baadhi ya kanuni za huduma za utangazaji 2005. Kamati ya maudhui inaamua kutoa onyo kali kwa Magic Radio, ” amesema na kuongeza.
“Pia inatakiwa kumuomba radhi Rais John Magufuli, wasikilizaji na wananchi kwa ujumla. Tangazo la kuomba radhi litolewe kwa siku tatu mfululizo katika taarifa za habari za saa 10.00 alasriri, na 3.00 usiku kuanzia tarehe 17,9,2016.”



Vituo hivyo ambavyo vilifungiwa na waziri wa Habari,utamaduni,sanaa na Michezo,Nape Nnauya kwa madai kuwa vituo hivyo kwa madai ya kutoa taarifa za uchochezi.
Waziri Nape alidai kuwa  kwa Mamlaka aliyopewa chini ya kifungu cha 28(1) cha sheria ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ya mwaka 2003 imempa mamlaka ya kuvifungia vituo hivyo,

Amesema Uamunuzi wa kuvifungia vituo amefikia baada kujiridhisha kuwa Redio five katika kipindi cha matukio kilichorushwa  tarehe 25 Agosti,2016 muda wa saa 2;00 usiku hadi saa 3;00 usiku  ambapo katika kipindi hicho alimuhojiwa Mbunge wa Arusha Majini,Godbless Lema ambapo alikuwa anatoa maneno anayosema ni uchochezi.
Amesema licha ya Mbunge huyo kutoa lugha hizo,lakini watangazaji wa kipindi hicho walishindwa kumsahihisha jambo analodai linakwenda kinyume na sheria ya utangazaji.
Mbali na Redio hiyo inayomilikiwa na Lowassa ambaye ni Alikuwa ni mgombea wa Urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kwenye uchaguzi uliopita pia ametaja kosa lilipelekea kukifungia kituo cha Magic Fm cha Dar es Salaam.
Amedai mnamo tarehe 17,Agosti 2016 katika kipindi cha Morning Magic kipindi hicho  kilichoruka mda  saa 1.00 asubuhi  na saa 2.30 katika kipengele cha Kupanga Rangi watangazaji wa kipindi hicho walisikiaka wakitoa maneno anayoeleza kuwa ni ya uchochezi.
“Watangazaji hawa Magic walisema kama Rais anavunja Katiba sasa wananchi wa chini wafanyaje,nao lazima watafanya hivyo,”Amesema Nape.

Waziri Nape alidai kuwa 

Endelea kufuatilia Fullhabari.bllogs habari kamili utapa