Zinazobamba

SHEIKH JALALA :RAMADHANI YA MWAKA HUU IWE DARASA LA HURUMA NA UPENDO



 
Kiongozi Mkuu wa chuo cha Kiislamu(HAWZA) Immam Swadiq Sheikh Hemed Jalala amewataka Waislamu na wasiokuwa waislamu kuitumia fursa ya mwezi Mtukufu wa Ramadhani kuachana na matendo yasiyompendeza Mungu na badala yake wajikite katika kuoneana huruma na kupendana miongoni mwao kwani kufanya hvyo ndiyo Mafundisho ya Mtume.

Akizungumza na Waandishi wa habari ofisini kwake, Kigogo Jijini Daresalaam wakati wa tukio la kuukaribuisha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, Sheikh Hemed Jalala amesema Mwezi wa Ramadhani unamafundisho mengi lakini kubwa watu wanapaswa kuoneana huruma na kupendana 

Amesema licha ya Ramadhani kuwa na Mafundisho mengi, kwa mwaka huu Jamii haina budi kuhakikisha wanaitumia Ramadhani kwa kuwaonea huruma wazee, mayatima, vikongwe na majirani zao kwani kufanya hivyo kutaongeza ustawi wa Amani miongoni mwa jamii.

“Funga ya mwaka huu naomba nifikishe ujumbe kuwa  iwe ni darsa la kuwahurumia mafakiri, mayatima na majirani zao nah ii ni kwa wote wawe Waislamu na wasio Waislamu, Wote tunajua anayefunga anaacha chakula chake anachopenda ili kuungana katika Ramadhani….ni somo la kufahamu mengi kuhusu wenzetu mafakiri, mayatima na wajane wanayopitia” Alisema Sheikh Jalala.

Katika hatua nyingine, wakati Nchi ikiwa katika sintofahamau kubwa kutokana na matukio ya mauaji ambayo yameitikisa nchi kwa kipindi kifupi na kuacha watanzania wakiwa katika wasiwasi Sheikh Jalala ametumia fursa hiyo kulaani vikali  mauaji ambayo ameyaita ya kiigaidi yaliyotokea katika mikoa mbalimbali nchini huku akisema kuwa vitendo hivyo vinakwenda kinyume na Imani ya dini yoyote nchini na vinastahili kupingwa na kila mtanzania.
 
Sheikh JALALA amesema kuwa Tanzania ni nchi iliyotambulika duniani kote kuwa kisiwa  ya Amani na utulivu hivyo vitendo hivyo ni vitendo ambavyo vinaharibu sifa ya nchi duniani kote.
 
Ameongeza kuwa vitendo vya ugaidi na ukatili pamoja na uvunjifu wa Amani nchini ni vitu vya kuwa makini sana na kuwa na tahadhari sana kwani vinaweza kuzuia hata waumini mbalimbali kuabudu kwa uhuru na Amani hasa kipindi hiku cha mfungo

Aidha amewataka watanzania sasa kuchukua jukumu la kuwa walinzi wa maeneo wanayoishi na kuhakikisha kuwa wanatoa taarifa haraka pale ambapo wanaona watu au kikundi cha watu ambao hawaeleweki wakiwa katika maeneo yao huku akivitaka vyombo vya usalama kuhakikisha kuwa wanachukua taarifa za wananchi na kuzifanyia kazi mara moja ili kuepuka kutokea kwa matukio ya kigaidi na mauaji kama yaliyotokea mwezi huu.

Tukumbuke kuwa siku za hivi karibuni kumekuwa na mfululizo wa matukio ya mauaji ya kutisha huku wengine wakichinjwa ambayo yaiyokea mkoani mwanza na mengine mkoani tanga matukio ambayo yameacha simanzi kwa watanzania walio wengi.

Hakuna maoni