Zinazobamba

MEYA WA UKAWA KINONDONI AWA MBOGO,AWASHUKIA WATENDAJI WANAOBALISHA HATI ZA VIWANJA,SOMA HAPO KUJUA



https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjP6apGIKEvRgTB9gWwZoYpt-ru733MYxV8wPR4wBcbWwII7WeYZAnxiUvkclwzNjb1jXZArRUo1K6eOdwqyFKD2wbaRkRC-vYHyuhV3gnr1fskqR0gdhw2qxk7OXo8tseJWRzQw3vWqgAW/s1600/WhatsApp-Image-20160606+%25286%2529.jpeg


Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Mhe. Boniface Jacob akiwaonesha waandishi wa habari ramani  inayoonyesha eneo la makaburi lililovamiwa na taasisi ya Mkapa Foundation ambalo limegaiwa na manispaa kinyume na taratibu.

 Kwa maelezo ya nyaraka za manispaa  zinavyoonyesha, eneo hilo limetolewa wakati baraza la madiwani likiwa limemaliza muda wake. Cha kushangaza eneo hilo, manispaa haijaambulia hata shilingi. Na mwisho kabisa mstahiki meya, ameaagiza kusimamishwa shughuli zozote katika eneo hilo.



MEYA  wa Manispaa ya Kinondoni,Boniface Jacob amewataka watendaji wa manispaa hiyo kuacha tabia ya kubadilisha hati za viwanja vilivyotengwa kwa ajili  maziko na kwenda kwa ajili ya matumizi ya  ujenzi wa majengo ya kawaida.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.

Jacob ameyasema hayo leo Jijini Dar es Salaam,wakati alipokuwa akifanya ziara ya kushtukiza kwenye eneo la Kawe jijini hapa ambao katika eneo hilo kuliibuka mgogoro mkubwa kati Wananchi wa eneo hilo –

Na  viongozi wa watendaji wa Kawe ambapo mgogoro huo ulitokana na eneo hilo kuwepo na kiwanja kilichokuwa kunatumiwa na wananchi hao kufanyiwa maziko ila kwa sasa kinadaiwa kuchukuliwa  na Taasisi ya Benjamini Mkapa Foudation kwa ajili ya kuendeleza huduma ya makazi ya Binadamu jambo lilowachukiza wananchi hao hadi kuifanya ofisi ya Meya kuingilia kati .

Jacob aliwataka watendaji wa manispaa hiyo  kuacha tabia ya kubalisha mtumizi  ya viwanja  vyote  ndani ya Kinondoni vilivyotengwa kwa ajili ya wananchi kufanyia maziko na kwenda kwenye ujenzi wa Makazi.

Amesema licha ya Manispaa hiyo kugubikwa na kashfa ya uuzwaji wa viwanja vya wazi vilivyotengwa kwa ajili ya michezo ila amesikitika na hali ya uuzwaji wa maeneo yalitoengwa kwa ajili ya Maziko jambo analodai linaichafua manispaa hiyo.
 

Meya huyo ambaye ni Diwani wa Kata ya Ubungo kupitia Chama cha Demokrasia na maendeleo Chadema amesema  kwa sasa hatakubali chini ya uongozi wake kuona wakazi wa kinondoni wananyanyashwa kwa kuanyang’anywa viwanja vyao pamoja na maeneo ya wazi kwa kusema atahakikisha maeneo yote yalioyotengwa kwa ajili ya huduma yanaendelezwa kwa huduma hizo.

Hakuna maoni