Zinazobamba

JESHI LA POLISI LAINGILIA KATI MAPAMBANO YA CHADEMA,ACT-WAZALENDO NA CCM,SOMA HAPO KUJUA



IGP Ernest Mangu , Mkuu Jeshi la polisi  Tanzania (wakwanza), Christopher Ole Sendeka, Msemaji wa CCM (Picha ndogo ya juu na  Benson Kigaila, Mkurugenzi wa Oganaizesheni, Mafunzo na Usimamizi wa Kanda (Chadema)(Picha ndogo ya chini)

JESHI la Polisi nchini limeingilia kati ‘vita’ ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na Chama Cha Mapinduzi (CCM), anaandika Faki Sosi.

Taarifa ya Nsato Mssanzya, Kamishna wa Polisi Operesheni na Mafunzo, Makao Makuu jijini Dar es Slaam imevunja mpango huo wa jino kwa jino kati ya CCM na Chadema uliotarajiwa kuanza leo.

CCM ilipanga kuingiza mguu sehemu ambayo Chadema itakuwa imeondoka. Ni baada ya kutangaza ziara ya kuzidua wananchi kuhusu haki ya kudai nchi kuendeshwa kwa mujibu wa Katiba.

“Jeshi la Polisi kupitia vyanzo vyake mbalimbali vya habari limebaini kuwa, mikutano hiyo ina lengo la kuwahamasisha wananchi kutotii sheria za nchi (Civil disorder),” imeeleza taarifa ya CP Mssanzya kwa vyombo vya habari.

Amekiri kwamba, jeshi hilo limepokea taarifa kutoka kwa baadhi ya vyama vya siasa wakitaka kufanya mikutano na maandamano.

“Kwa hali hiyo, Jeshi la Polisi nchini linapiga marufuku maandamano na mikutano ya hadhara kuanzia tarehe 07/06/2016 hadi hapo hali ya usalama itakapotengemaa.

“Jeshi la Polisi linawataka wanasiasa kuacha mara moja kuwashinikiza wananchi kutotii sheria za nchi.  Jeshi la Polisi halitasita kumchukulia hatua kali za kisheria mtu yeyote au chama chochote cha siasa kitakachokaidi agizo hili,” imeeleza taarifa hiyo.

Hivi karibuni Chadema kupitia kwa Benson Kigaila, Mkurugenzi wa Oganaizesheni, Mafunzo na Usimamizi wa Kanda alitangaza kuanza kwa ziara ya chama hicho.

Akizungumza na waandishi wa habari Kigaila alisema, lengo la ziara hiyo ni kukumbusha wananchi kwamba, nchi inapaswa kuendeshwa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri.

Alidai Rais John Magufuli anaendesha nchi kinyume na taratibu pia Katiba ya Nchi na kwamba, ziara hiyo imepangwa ili kuzindua wananchi wajibu wa kudai viongozi waongoze kwa mujibu wa Katiba ya Nchi.

Ziara hiyo ilipangwa kuanza kutekelezwa tarehe 7 Juni mwaka huu nakuanzia mkoani Shinyanga, Wilaya ya Kahama.

Na baada ya hapo kutakuwa na timu mbili zitakazozunguka katika mikoa yote nchini ikiwemo ya Chato, Bukoba, Geita, Sengerema, Muleba, Meatu, Bunda, Bariadi na kumalizika Mwanza ambapo timu hizo mbili zitakutana.

“Tangu kuingia madarakani Rais Magufuli kumekuwa na ukiukwaji wa sheria na katiba, serikali imekuwa ya mtu mmoja na maamuzi ya mtu mmoja kana kwamba, hakuna wizara husika kitu ambacho kinawakandamiza wananchi na kushindwa kupata haki zao,” amesema na kuongeza;
“Hatuta choka kupiga kelele anapoenda kinyume na kupuuza Katiba ya nchi na tunataka wananchi wa mtambue na wajue namna ya kudai haki zao. Tangu kuingia kwake madarakani hakuna maendeleo zaidi ya kulipiza visasi kwa watu ambao hawakumuunga mkono wakati wa kampeni.
“Rais Magufuli amevunja na kuvuruga vitu vingi vilivyopo kwenye Katiba ikiwepo sikukuu, kupanga matumizi ya fedha wakati wizara husika zipo, uvurugaji wa bunge na mengine mengi yasiyomuhusu,” alisema Kigaila.
Baada ya kauli hiyo, Christopher Ole Sendeka, Msemaji wa CCM alisema kuwa, chama chake hakitokalia kimya chochote kitakachoonekana kuipaka matope CCM pia Rais Magufuli anayetokana na chama hicho.
Ole Sendeka alinukuliwa akisema kuwa, Chadema kinataka kufanya ziara hiyo kwa ajili ya kuishitaki Serikali ya Rais Magufuli kwamba ni ya kifashisti na kidikteta.
“Kuanzia Mei 6 mwaka huu baada ya Kikao cha Kamati Kuu ya Chadema habari zilianza kuandikwa na gazeti moja la kila wiki kuhusu mikakati ya chama hicho.
“Pia ziliandikwa makala zikieleza yale yaliyojiri kwenye kikao cha kamati kuu kwamba watakwenda kuishitaki  Serikali Rais Magufuli kuipeleka nchi kifashisti na inaongozwa kidikteta…,
“Mambo haya yamekuwa yakirudiwa mara kwa mara si vema kuyanyamazia,” alinukuliwa Ole Sendeka akidai kwamba, kwake tatizo zi mikutano isipokuwa maudhui yake.
“Kama wataenda kuyasema mambo kama haya wakitoa mguu nami naweka mguu wangu kueleza wananchi jinsi Chadema inavyotetea mafisadi,” amesema Ole Sendeka.
Katika taarifa ya Jeshi la Polisi imeeleza kuwa, chama chochote hakiruhusiwi kufanya mikutano mpaka pale taarifa mpya itakapotolewa.
·                      
·                     25
·                     1
·                      
·                      
·                      

Hakuna maoni