Zinazobamba

ANNA MGHWIRA WA CHAMA CHA ACT-WAZALENDO ATOA NENO TUHUMA ZA WABUNGE KUTOA RUSHWA YA NGONO KUPATA UBUNGE,SOMA HAPO KUJUA


Pichani ni Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo,Anna Mghwira (picha na Maktaba)

Mwenyekiti wa chama cha ACT-Wazalendo Anna Elisha Mghwira amekili kuwepo kwa vitendo vya rushwa na ngono katika mchakato wa kuwapata wabunge wa viti maalamu ndani ya vyama vyao nchini.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.

Mghwira aliyasema hayo mwishoni mwa wiki  jijini dar es salaam katika kongamano la wanawake ,katiba na uchaguzi lililoandaliwa na mtandao wa wanawake nchini lenye lengo la kujadili fursa ,changamo,pamoja na matazamio ya nafasi ya ubunge wa viti maalumu nchini.

Bi Mghwira  ambaye alikuwa mgombea Rais  pee mwakanamke katika uchaguzi mkuu wa mwaka jana alisema vitendo hivyo vinasababishwa na wanawake wenyewe kutokujiamini pindi wanapoomba nafasi za kugombea  na kutegemea msaada kutoka kwa wanaume licha ya wenyewe kuwa na uwezo wa kusimama mwenyewe.

“Hata tukiondoa viti maalumu rushwa ya ngono itaendelea kuwepo nchini endapo wanawake tutashindwa kujitambua pamoja na kusimama wenyewe”Amesema Mghirwa.

Kwa upande wao washiriki katika kongamano hilo wamevitaka vyama kubadili  mfumo wa sasa wakuwapata wabunge wa viti maalumu pamoja na kuitaka jamii kubadili fikra za kila mwanamke aliyefanikiwa kuwa amewetumia rishwa ya ngono kupata nafasi hiyo.

Aidha wamesema rushwa ya ngono haitaisha nchini kutokana na wanawake kupenda watu wenye vitu pamoja na wanawake wengi kutojiamini katika kushughuli zao.

Naye Mkurugenzi wa Mtandani wa Kijinsia kutoka TGN,Lilian Liundi aliwataka wanawake kujiamini na kuachana na kasumba na kujuaminisha kuwa  kila nafasi ya uongozi ndani ya nchi inapatikana kwa kutua rushwa ya Ngono.

Be Liundi amesema kwa sasa Jamii inatakiwa kuondoa dhana potofu kwa wanawake ambayo inamchukulia mwanamke ni kiumbe dhaifu kwa kudai kuwa mwanamke ni mtu mwenye maono ambayo yanaweza kuibadilisha jamii.


Hakuna maoni