Zinazobamba

WATETEZI WA HAKI ZA BINADAMU WALAANI WANAURUSHA PICHA CHAFU MTANDAONI




Mkurugenzi Mtendaaji wa kituo cha sheria na haki za Binadamu Nchini Tanzania LHRC Bi Hellen Kijo Bisimba akizungumza na wanahabari mapema leo

Mashirika yanayofanya kazi ya utetezi wa haki za binadam hasa zinahusu makundi maalum ya watoto na wanawake wamejitokeza na kulaani vikali vitendo vya kuchapisha picha na video chafu katika mitandao ya kijamii.
Akizungumza na Waandishi wa habari mapema hii leo kwa niaba ya watetezi hao, Mkurugenzi wa kituo cha sharia na haki za Binadamu Bi Kijo Bisimba amesema hivi sasa watu wamekuwa wakitumia mitandao ya facebook,instagram,blog na whatsapp kutupia picha mbalimbali zinazokwenda kinyume na maadili ya Kitanzania
Amesema picha nyingi zinazorushwa katika mitandao zimekosa maadili, utu,na zimekuwa zinaingilia faragha za watu jambo ambalo linakwenda kinyume na katiba ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania sambamba na kukiuka haki za binadamu.

Ametaja baadhi ya matukio ambayo yamesambazwa katika mitandao ya kijamii lakini yamekiuka maadili ni pamoja vifo vya mama na motto kilichotokea Bagamoyo mnamo tarehe Mei 4,2016 ambapo picha zilipigwa na kuonyesha miili ya marehemu ikiwa na majeraha ya kutisha kwa kitendo walichofanyiwa.

Tukio lingine ni lile lilitokea Mkoani Kilimanjaro ambapo mtoto alipigwa picha na kuzituma katika mitandao ya kijamii zikimuonyesha akiwa katika jeneza baada ya kuuwawa na mama yake wa kambo.

Mbali na tukio hilo pia, DKT Bisimba amesema wamesikitisha na tukio la kumuonyesha utupu wa mtu mmoja aliyedaiwa kuwa Msukule baada ya kukutwa katika kisima kimoja huko Kibamba  jijini Daresalaam na kusema si maadili kuonyesha utupu wake.
“Chukulia kuwa yule ni mama yako Dada yako amekutwa hivyo na kupigwa picha za utupu ungejisiakije, lazima watu wabadilike na serikali ichukue hatua katika masuala haya”Alisema Bisimba.

Katika hatua nyingine, Bi Bisimba ameitaka jamii kuacha kabisa tabia ya kuwavunjia makundi ya watoto na wanawake kwani picha zinazorushwa katika mitandao zinawaathiri wahusika na kuchochea maumivu ya kihisia kwake na ndugu wa familia yake.

Aidha kwa upande wa Serikali, watetezi hao wa haki za binadamu wameitaka serikali ichukue hatua kali za kisheria kwa wanaotumia mitandao vibaya bila ya kujali vyeo vyao.



Wanahabari wakiwa kazini
 
 

Hakuna maoni