Zinazobamba

WAFANYABIASHARA WA KARIKAOO MWISHO MEI 8,NI WALE WANAOFANYA BIASHARA BARABARANI,SOMA HAPO KUJUA


kariakoo
Pichani ni Wafanyabiashara wa Kaliakoo ambao wanatakiwa kuondoka Kabla ya Mei 8 mwaka huu


HALMASHAURI ya Manispaa ya Ilala imewataka wafanyabiashara wote wanaofanya biashara katika maeneo yasiyo rasmi wawe wameondoka kwenye maeneo hayo kabla ya mei 8 mwaka huu,lasivyo halmashauri hiyo itawachua hatua za kinguvu kuwaondoa katika maeneo hayo.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo

Akitangaza uamuzi huo,mbele ya Waandishi wa habari jijini Dar es Salaam,Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, saya Mnguruni amesema wanafanyabiashara wanatakiwa kuodoka kwenye maeneo hayo kutokana na   halmashauri hiyo kutenga maeneo maalum yenye huduma stahiki kwa wafanyabiashara hao zaidi ya 2961,

Mnguruni ameyataja  maeneo hayo  yaliyotengwa ni pamoja na Tabata Muslim, Ukonga, Kivule, na Kigogo Fresh.

Mkurugezi huyo amebainisha kuwa  maeneo hayo yaliyotengwa yanauwezo wa kuchukua wafanyabiashara zaidi ya 6000 na yana huduma zote stahiki huku akiongeza kuwa maeneo hayo yatawekewa vituo vya daladala ili yaweze kufikika kiurahisi.


No comments