Zinazobamba

TAZARA BADO HALI TETE,YAKABILIWA NA CHANGAMOTO HIZI,SOMA HAPO KUJUA



Wasafiri wakiwa katika foleni kuingia kwenye

SHIRIKA la Reli la Tanzania na Zambia (TAZARA) linakabiliwa na Changamoto za Rasilimali watu pamoja na mitaji ya fedha ambapo changamoto hizo zimepelekea  shirika hilo kutofikia malengo yake.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo

Hayo yamesemwa leo Jijini Dar es Salaam na Kaimu mkurugenzi  mkuu wa (TAZARA) Dkt Betram Kiswaga wakati wa uzinduzi wa kitabu kinachozungumzia histori ya shirika hilo tangu lianza kufanya kazi kwenye miaka ya 1970 ambapo kitabu hicho kimeandaliwa na nchi ya China ambao ndio waliotengeneza reli kutoka Tanzania hadi Zambia.
 
Dkt Kiswaga amesema TAZARA linashindwa kwenda na kasi ya ufanyaji kazi ambao ungeweza kuliingizia taifa mapato.
Kiswaga amefafanua kuwa kutokuwepo na rasilimali watu wenye sifa na utaalamu  kumechangia shirika hilo kushindwa kujiendesha vizuri.

“Nina mwaka mmoja kwenye Tazara ila shirika hili limeshiindwa kufanya kazi kama tunavyotaka kutokana kutokuwa na wataaalumu wenye sifa huku wengi wakiacha kufanya kazi na Tazara kutokana na shirika kutokuwa na mitaji ya fedha ambayo ingeweza kuwamudu wataalamu”amesema Dk Kiswaga.

Hata hivyo,Dk Kiswaga amesema licha ya kukumbuna na changamoto hizo,amedai bado shirika hilo linaendelea na kutoa huduma ya usafiri kutoka Tanzania na Zambia huku akitoa Pongezi kwa nchi ya China kuendelea kutoa ushirikiana kwa shirika hilo.
Naye Balozi wa China nchini LU Youqing  amesema Serikali ya China itaendelea kutoa ushirikiana kwa shirika hilo.

Amesema kwa sasa wanafahamu shirika hilo linakumbana na changamoto jambo analodai kuwa nchi yake hatosita kulisaidia shirika hilo katika  kuzitatua changamoto hizo.

Hakuna maoni