Zinazobamba

CHAMA CHA CUF CHAFICHUA SIRI NZITO YA UBAGUZI NA CHUKI UNAOENDELEA ZANZIBAR,SOMA HAPO KUJUA



 Twaha Taslima, Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi wa Chama cha Wananchi (CUF) Taifa (Kushoto), Maalim Seif Sharif Hamad aliyekua mgombea Urais Visiwani Zanzibar (CUF) (Kulia).

UKANDAMIZWAJI wa demokrasia unaofanywa na serikali ya awamu ya tano ndiyo chanzo cha ubaguzi na chuki iliyopo miongoni mwa wananchi wa visiwani Zanzibar, anaandika Regina Mkonde.

Hayo yamesemwa leo na Twaha Taslima, Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi wa Chama cha Wananchi (CUF) Taifa wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

“Katika matukio ya kukanyaga demokrasia madhara yake ni kujenga chuki na ubaguzi kwa watanzania dhidi ya serikali yao na kwamba hali hii itasababisha vurugu na kuathiri maendeleo ya nchi kutokana na uwepo wa muendelezo wa chuki,” amesema Taslima.

Taslima amesema kuwa serikali ya awamu ya tano inaonesha dhahiri kwa matendo yake kwamba haina  mpango na haitaki demokrasia na kwamba mkakati wake ni kuendelea kukandamiza demokrasia.

“Serikali inadhani kuwa kuendelea kukandamiza kutasaidia wao kubaki madarakani zaidi na zaidi jambo ambalo wanajidanganya,” amesema.

Licha ya ukandamizwaji wa demokrasia, Taslima  amesema CUF imeshuhudia ukandamizwaji wa haki ya wananchi ya kupata habari na kuhabarisha kutoka na kwamba wanahabari wanatishwa na kukandamizwa wasitoe taarifa kwa uhuru.

“Mfano mzuri ni kutekwa kwa Salma Saidi, mwandishi wa DW Zanzibar, na kile kitendo cha wananchi kuziwa kupata taarifa wanazopaswa kupata kama vile kuundwa na kutekelezwa kwa sheria kandamizi ya matumizi ya mtandao,” amesema.
Aidha, amesema kuzuiliwa kwa matangazo ya moja kwa moja ya bunge hatua iliyofanywa na serikali ya awamu ya tano imelenga kuficha wananchi shughuli zinazofanywa na wawakilishi wao.
Kuhusu kauli iliyotolewa na Kasim Majaliwa, Waziri Mkuu akiwa London nchini Uingereza baada ya kuulizwa swali kuwa kwa nini serikali ya awamu ya tano hairushi matangazo ya bunge live.
Na kujibu kuwa sababu ni watanzania kutopenda kufanya kazi wakati wa matangazo hayo yanaporushwa kwa kuwa hupoteza muda wao kuangalia bunge, Taslim amemtaka Waziri kuomba radhi watanzania.
“Waziri Mkuu bila aibu alisema kuwa wataznaia hawapendi kazi na wanakuwa wanaangalia bunge muda wote badala ya kufanya kazi, hii kauli ni ya kidhalilishaji sana kwa watanzania,” amesema.
Taslima amesema hiyo siyo hoja kutokana n akwamba kama watanzania wangekuwa wanaangalia bunge live muda wote maendeleo na maisha yao wengi yangekwama.
“Si kosa wananchi kufuatilia bunge kwa kuwa mwananchi yeyote makini anafuatilia taarifa za masuala mbalimbali ya nchi kwani maamuzi yanayojadiliwa na kuamuliwa bungeni yanaathiri maisha yao pia inatoa mwanya kwa wananchi kupima serikali yake kama inatekeleza majukumu yake,” amesema.
Amesema, serikali ni lazima ikaangalia upya na kufuata misingi ya demokrasia , haki za wananchi kwa sababu haki inaponyimwa husababishwa kutoelewana baina yao.
“Serikali kazi yake kubwa hivi sasa ni kutaka kuwarudisha nyuma wananchi kwenye uwoga wa kutoiwajibisha serikali eti kwa kisingizio cha hapa kazi tu, aweamu ya tano inakuja na slogan ya hapa kazi tu ya kuua demokrasia,” amesema

Hakuna maoni