BURIANI DIWANI WA KIJICHI ANDERSON CHALE,
Mkuu wa Polisi Mkoa wa Temeke,RPC Kamishina Msaidizi, Gilles Muroto,akisalimiana na Aliyekuwa Diwani wa Kurasini (CCM),Wilfred Kimath baada ya kuongozana na Mkuu wa Wilaya ya Temeke,Sophia Mjema (katikati) kwenda kutoa pole nyumbani kwa marehemu.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke,Sophia Mjema,akisikiliza kutoka kwa ndugu wa marehemu chanzo cha msiba wa marehem,u ambacho ni mshituko wa moyo.
Aidha binamu wa Marehemu aitwaye Anna Komba,alisema kuwa Marehemu Diwani wa Kata ya Kijichi,Anderson Chale alipatwa na mshituko wa moyo kwa taarifa ya hospitali kwa kuwa kabla ya hapo awali alikuwa ana tatizo la Presha na ratiba ya mazishi ni kwamba mwili wa marehemu utasafirishwa jumatano kuelekea nyumbani kwao Liuri,Wilaya ya Nyasa,mkoani Ruvuma kupumzishwa kwenye nyumba yake ya milele.
Wakazi wa eneo hilo wakiomboleza
Baadhi ya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakiwa kwenye msiba huo
Mkuu wa Wilaya ya Temeke,Sophia Mjema,akitoa pole kwa ndugu
wa aliyekuwa Diwani wa Kata ya Kijichi CCM,Anderson Chale,aliyefariki dunia
juzi kwa mshituko wa moyo,nyumbani kwake,Kijichi,jijini Dar es Salaam,leo. Picha zote na Elisa Shunda
Baadhi ya wananchi waliohudhuria katika msiba huo nyumbani kwa marehemu kijichi
Mkuu wa Wilaya ya Temeke,Sophia Mjema na msafara wake wakiondoka katika eneo hilo baada ya kutoa pole kutoka ofisi ya Wilaya ya Temeke.
Muonekano wa Nyumba ya Marehemu aliyokuwa akiishi eneo la Kijichi,wilayani Temeke,Dar es Salaam
Hakuna maoni
Chapisha Maoni