Zinazobamba

KUBWA-AZAM MEDIA YAIBOMOA BBC YAMCHUKUA KIFAA WAKE MUHIMU,WAAPA KUZOA WENGI SOMA HAPA KUJUA

Wafanyakazi wa Shirika la Utangaza la uingereza
 BBC wakimuaga na kumpatia jezi ya Mpira
 Charles Hillary juzi nchini Uingereza

MTANGAZAJI maarufu wa Shirika la Utangazaji la uingereza (BBC) Charles Hillary  hatimaye ameacha kazi kwenye shirika hilo na kujiunga rasmi na Azam Media.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo

 

      Charles Hillary ambaye amejipatia umaarufu mkubwa barani  Afrika na maeneo mbalimbali duniani kwa ustadi wake wa kutangaza mechi za mpira wa miguu yaani soka kwenye maeneo mbalimbali hususani  ligi za ulaya na Afrika ambapo sasa amejiunga na Azam media na kupewa mkataba mnono.

 

     Kwa mujibu wa mtoa taarifa wetu aliyoko kwenye Kampuni ya Azam Media ambayo inamilikiwa na Mfanyabishara mkubwa hapa nchini bwana Said Salim Bakhresa zinasema mtangazaji huyo atachukua nafasi ya Tido Muhando katika kuendesha kampuni hiyo ambapo sasa Tido muhando atakuwa chini yake.

 

       Azam Media ambayo hivi karibuni wamefungua studio za kisasa kabisa zilizoko Tabata Relini Jijini Dar es Salaam ambazo zimegharimu zaidi ya Bilioni 54 pesa  za kitanzania,Taarifa zainadai kitendo cha Mfanyabiashara huyo kumleta Charles Hillary ni kutaka kuboresha maudhui ya vipindi vya runinga hiyo viendane na ubora wa Studio zake zilizopo sasa.

 

        Charles Hillary ambaye juzi teyari alikuwa ameshawaaga wafanyakazi wenzake waliokuwa wanafanya kazi pamoja huko BBC na kuwahakikisha kujiunga na Azam media.

        Chanzo chetu hicho kilichopo Azam Media kinadi kwamba kuja kwa Hillary sio mwanzo tu kwani mfanyibiashara huyo amepaniwa kuwachukua watangazaji wengi na wenye uwezo ambapo anasema sio nchini tu hadi kwenye nchi yeyote nia kuleta mapinduzi ya vyombo vya Habari hapa nchini na Afrika kwa Ujumla.

    Kabla ya kuja na Charles Hillary hapo Azam tayari kampuni hiyo ilikuwa imewachukua waandishi na watangazaji nyota kwenye tasnia ya vyombo vya Habari nchini na kwengineko.

 

   Watangazaji hao ni Tido Muhando ambaye alikuwa Mhariri Mtendaji wa Gazeti la mwananchi, Baluani Muuza  ambaye naye alikuwa mwakilishi wa BBC Swahili Afrika kutoka Dar es Salaam,pamoja na watangazaji wengine kutoka nchini.

      Kampuni ya Azam media kwa sasa ndio kampuni ya kipekee iliyopewa idhini ya kurusha moja kwa moja ligi ya Tanzania Bara.

     Mbali ya ligi hiyo kampuni hiyo imeshangia katika nchi jirani ikiwemo na Uganda na Burundi na kupewa idhini ya kurusha moja kwa moja ligi za nchini umo.

   WADAU WA HABARI WANENA.

Wadau mbalimbali na wachambuzi wa masuala ya Habari waliozungumza na mwandishi wa mtandao huu wamesema kitendo cha Charse Hillary kuhamia Azam media kutaleta mafanikio makubwa katika Nyanja ya habari nchini kutokana na weredi wake aliounyesha huko uingereza,\.

No comments