Zinazobamba

HABARI KUWA,SAMWEL SITTA ACHARUKA,AWASIMAMISHA VIGOGO TRL,WAMEITIA HASARA BILION 230 SERIKALI,SOMA HAPA KUJUA

WAZIRI wa Uchukuzi Samwel Sitta (pichani) amewasimamisha Kazi Vigogo wa Juu wa Mamlaka ya  Reli ya kati nchini TRL kutokana na kuitia hasara Serikali inayofikia Bilioni 230 kwenye ununuzi wa mabehewa ambayo yamebainika ni ‘Feki’Anaripoti KAROLI VINSENT endelea nayo.
      Watendaji hao waliosimamishwa kazi ni Mkurugenzi Mtendaji Kipallo Kisamfu,Mhandisi mkuu wa mitambo Ngosowile Ngosomiles,Mhasibu Mkuu  Mbaraka Mchopa,
     Wengine ni Mkaguzi mkuu wa ndani wa Kampuni Jasper Kisiraga,pamoja Meneja Mkuu wa Manunuzi Fedinard Soka.
         Akitangaza uamuzi huo mda huu Jijini Dar es Salaam Waziri wa Uchukuzi Samweli Sitta wakati wa mkutano na waandishi wa habari ambapo amesema baada ya kupokea ripoti ya Tume iliyoundwa na waziri aliyekuwepo kwenye wizara hiyo Harrison mwakyembe na kumkabidhi ripori imeonyesha mabehewa hayo ni mabovu hayafai kutumika kupakia Abiria.
        “Baada ya kupata Ripoti hii tumejidhilizisha wazi kwamba mabehewa haya ni mabovu na hayafai kutumika kabisa tena mengi yanakasoro kubwa na hayawezi kutembea kabisa na nilipogundua mabehewa haya ni mabovu nikayazuia ”Amesema Waziri
         Waziri Sitta ameongeza kuwa licha ya kuzuia uigizaji wa mabehewa hayo jambo ambalo  anadai limemshangaza ni kitendo cha watendaji hao kutoa kutoa pesa zote kwenye kampuni inayotengeneza mabehewa hayo kinyume na taratibu za umma.
     “Yaani waandishi wa Habari nimeshangaza sana na hujuma ambayo inafanywa na watendaji hawa wa Reli ambayo sitegemea kabisa na siwezi kufumbia macho maana unapoipa tenda kampuni itengeneza na Mabehewa na kuyaleta inatakiwa utoe pesa kwa mafungu,yaani hatua ya kwanza unatoa asilimia 40 ya fedha”
      “Kabla ya hatua ya pili unatoa fedha baada ya kuyapokea mabehewa nusu na hatu ya pili sasa unatoa asilimia 40 tena mabehewa yanakuwa yemekuja yote na asilimia 20 inatoa baada ya kuyajalibu mabehewa yanafika yanatembea vizuri hadi kigoma au la,sasa jambo la kushangaza watendaji hawa hawajafuata kanuni hizo wametoa pesa zote Bilioni 230,wakati ni tofauti kabisa na sheria za Serikali”ameongeza Waziri Sitta
          Aidha, Waziri Sitta amesema baada ya kubaini hali hiyo ndipo amechukua hatua ya kusimamisha watendaji hao kupisha tume ya uchunguzi iwachunguze kutokana kuvunja kununi kwa  kutoa fedha zote.
        “Baada ya kubaini hawa watendaji wamefanya uzembe huu nimewasimamisha kazi,ili kupisha uchunguzi wa kamati,ambayo inayoundwa na kukushirikiana Ofisi ya kupambana na rushwa (TAKUKURU),Ofisi ya Mwanasheria Mkuu,Mamlaka ununuzi katika sekta ya Umma (PPRA),wizara ya Uchukuzi pamoja na ofisi ya mkaguzi mkuu wa Hesabu ya Serikali (CAG) na nimeipa wiki tatu iwe imekamilika kuchunguza Uzembe huu”amesema Waziri Sitta.
         Vilevile Waziri Sitta amesema kwa sasa ameitaka Bodi ya Wakurugenzi Kampuni ya Reli ikae kikao cha Dharura kwaanzia kesho na  kuteua watendaji wengine kuziba nafasi zao.
         Katika hatua nyingine Waziri wa Uchukuzi Samwel Sitta amemuondoa kabisa katika nafasi aliyokuwa amesemamisha Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bandari Bwana Madeni Kipande baada ya Tume aliyoinda kumaliza kazi yake.
     Waziri Sitta amesema kwa mujibu wa  Ripoti ya tume hiyo imebaini mkurugenzi huyo kushindwa kabisa kuisimamia Bandari hiyo na kusababisha matatizo kwa wateja.
       “Baada kuisoma taarifa ya tume na hatimaye kushauriana na taasisi mbali mbali zinazohusika na masuala haya,tumeridhika pasipo mashaka ndugu kipande afai kuongoza mamlaka hii ya bandari kutokana na kutokuwa na sifa tena amesababisha matatizo”
         Amebainisha kuwa kwa sasa nafasi hiyo itaendelea kushikwa na Awadh Massawe,na huku bwana kipande akirudishwa Wizarani hapo kutafutiwa kazi nyingine.


No comments