Zinazobamba

DC MAKONDA ACHARUKA ,AUNDA TUME KUCHUNGUZA MADUDU KINONDONI,SOMA HAPA KUJUA

    

MKUU wa wilaya ya Kinondoni Paul Makonda (pichani)ameunda tume ya watu wa tano kuchunguza malalamiko ya Wananchi juu ya Ubovu wa barabara na miundombinu mingine ambazo zinadaiwa kujengwa chini ya kiwango.Anaandika KAROLI VINSENT,Endelea nayo.
           Hayo yamesemwa na Makonda leo Jijini Dar es Salaam wakati na mkutano na Vyombo vya Habari ambapo amesema tangu akabidhiwe nafasi hiyo amekuwa akipata malalamiko mbalimbali kutoka kwa wakazi wa wilaya ya Kinondoni juu ya Ubovu wa barabara ambapo Wakazi hao walikuwa wakisema barabara hizo zinajengwa chini ya kiwango.
           “Yaani wananchi wanasema barabara zinaubovu mkubwa,kwa kiasi Lami inawekwa leo lakini haimalizi miezi Sita inabanduka na inaacha mashimo,Mitaro inachimbwa mifupi kuliko mahitaji halisi,barabara zinakuwa nyembamba kutoka kushoto kwenda kulia,yaani wananchi wanaona kwamba hakuna serikali ya kuona hali hii”amesema Makonda.
       Makonda ameongeza kuwa baada ya kupata malalamiko hayo,yeye kama kiongozi wa serikali amesema haoni haja ya kuacha uzembe huo,na ndio maana ameamua kuunda tume ya watu mbalimbali wa masuala ya ujenzi kuchunguza malalamiko hayo ndani ya siku 21 na akabidhiwe ripoti kamili.
          Aidha,Makonda aliwataja watu katika tume hiyo ni Enginia Julius Mamilo ambaye atakuwa mwenyekiti wa Tume hiyo,Enginia Ronald Rwakatare naye pia atakuwa Katibu.
        Mbali ya Viongozi hao watume DC  Mkonda aliwataja wajumbe wa Tume hiyo ni John Malisa,Abednego Lyaga pamoja na Enginia Patrick Balozi.

        Kwa mujibu wa Makonda anasema pindi atakabidhiwa ripoti huyo atachukua hatua kali ikiwemo kuwafukuza kazi watendaji waliohusika na uzembe huo. 

No comments