KUBWA-MCHUNGAJI MSIGWA ARUSHIA KOMBORA SERIKALI YA KIKWETE,SOMA HAPA KUJUA
NA KAROLI
VINSENT
MBUNGE wa Iringa Mijini (CHADEMA) Mchungaji Piter
Msigwa ni kama ameishukia serikali ya Chama cha mapinduzi CCM inayoongozwa na
Rais Jakaya Kikwete na kusema ni Serikali hatari ambayo haitakiwi kupewa nafasi
tena, kutokana kuzidisha anaodai ni utendaji mbovu na kuwaacha wananchi wakilalamika
na maisha magumu.
Vilevile Mchungaji Msigwa amesema pia Rais Kikwete asiwakemee viongozi
wa dini pindi wanapoikataa Katiba iliyopendezekwa na Bunge Maalum la Katiba
kutokana na katiba hiyo kujaa ghiliba nyingi pamoja na ubabe kwenye upitishaji
wake ambapo anadai kiongozi wa kweli wa dini hawezi kuruhusu hali hiyo.
Kauli ya Mchungaji Msigwa ameitoa leo
wakati alipokuwa anahojiwa na kituo cha Redio cha Magic FM katika kipindi cha
Morning Magic ambapo amesema kwa sasa Taifa limekosa dira kutokana na Viongozi
waliopo madarakani kuzidisha undugu yaani anadai ndio unaochangia watanzania kuwa masikini wa kutupwa.
Mchungaji Msigwa ambae ni Waziri
Kuvuli wa Maliasili na Utalii amendelea kusema hata hali ya sasa ya Viongozi wa
dini kutoa matamko mazito kuhusu mambo mbalimbali ya nchi ni ishara ya wazi
tayari viongozi hao wameshaichoka Serikali iliyoko madarakani.
“Nani asiyejua kwamba mwanzoni
viongozi hawa dini walikuwa upande wa Serikali ya CCM,lakini leo wameona wazi
kwamba Serikali hii haina tija na imejaa uhasama ndio maana wao wameamua
kuwahasa waumini hao kuyakataa mambo mabaya na kiongozi wa dini lazima afanye
hivyo”ameongeza Mchungaji Msigwa.
Aidha, Mchungaji Msigwa amesema
kuwa kitendo cha Rais Jakaya kikwete kuwatupia lawama viongozi wa dini kwa
vitendo vyao vya kuwafosi waumini wao kuikaa Katiba pendendekezwa,ni kutaka
huruma kwa viongozi wakiroho.
“Namshanga sana anavyosema viongozi wa dini kuwafosi waumini wao
kuikataa katiba hiyo,wakati yeye mwenyewe amesahau kwamba alitumia idara zake
mbalimbali za Serikali ikiwemo TBC kuwataka wananchi waipigie ya ndio lakini
hilo halikuona lakini leo analiona la viongozi wa dini,ukweli katiba ile ni
mbovu”amesema
No comments
Post a Comment