BREAKING NEWS-NAULI ZA MABASI ZASHUKA,WAGOMA KUSHUSHA MENGINE KISA USUMBUFU WA CHENJI,SOMA HAPA KUJUA
MAMLAKA ya
Udhibiti Usafiri wa nchi Kavu na Majini nchini (SUMATRA) imeshusha Nauli kwa
kiwango kidogo kwa wasafiri kwa Masafa marefu yaani kutoka mkoa moja hadi mkoa mwengine kwa asilimia 7.8.Anaandika KAROLI VINSENT endelea
nayo
Vilevile Mamlaka hiyo imegoma kushusha
nauli za ndani ya mikoa husika, baada ya kubaini kiwango kilichoshushwa cha Shilingi 25 toka kwa nauli iliyopo sasa ambayo wanadai italeta usumbufu kwa Abaria
na Wamiliki wa Mabasi.
Hayo yamesemwa Mda huu Jijini Dar es
Salaam na Mkurugenzi mkuu wa (SUMATRA) Gilliard Ngewe wakati akizungumza na
waandishi wa Habari ambapo amesema hatua hiyo imetokana na maamuzi ya Bodi ya
Sumatra kufanikisha zoezi la ukokotoaji ambao anasema ukotoaji huo uliangalia
mambo mawili ya msingi yaliyosemwa na wadau wa Usafilishaji.
Mambo hayo ni Kushuka kwa Mafuta kwenye masoko
mbalimbali na kushuka kwa kodi ya Uingizaji wa Magari mapya ya Usafilishaji
nchini.
“Baada ya kuangalia
vigezo hivyo baraza ililifikia hatua ya kushusha nauli za mabasi ya ndani
yanayofanya shughuli zake katika mkoa husika kwa shilingi 25,ila baada ya
kushauliana tukaoni kushusha kwa kiasi hicho kitaleta usumbufu na kwa wateja,na
tukafikia uamuazi wa kuacha nauli za mwanzo itumike’
"Nahapa
tumeshusha nauli za mabasi ya masafa marefu tena yakutoka mkoa mmoja kweda
sehemu nyingine ,”amesema Ngewe
Aidha,Amesema kulingana na ukokotoaji
wa Nauli hizo Mamlaka hiyo imezingatia Kanuni za huduma za Abiria zinazoainisha
Aina nne ya Madaraja ya Mabasi.
Hata hivyo amesema kuwa viwango hivyo
vipya vitaanza kutimika kwaanzia rasmi tarehe 30 Aprili mwaka huu,na akawata
wamiliki wa Mabasi pamoja na Wafanyakazi wake kutoza Viwango vya Nauli
vilivyotolewa na Mamlaka usika.
Viwango vya
Nauli kutokana na Ukotoaji vya Mabasi ya ndani ya mkoa usika ambapo ukokotoaji
wa viwango vipya,Sumatra imeacha nauli zinazochajiwa kwa sasa kama unavyoona hapo, zitumike kutokana na viwango vipya vya nauli iliyokotolewa ya pungufu la shiringi 25
ingeleta usumbufu kwa Abiria,soma hapo,
ingeleta usumbufu kwa Abiria,soma hapo,
Njia
|
Nauli
ya sasa
|
Nauli
iliyokokotolewa
|
0-10
|
400
|
376.77
|
11-15KM
|
450
|
448.62
|
16-20km
|
500
|
465.34
|
21-25km
|
600
|
583.34
|
26-30 km
|
750
|
742.74
|
Daraja la basi
|
Nauli
ya sasa
TZS
/Abiria km
|
Viwango
vipya vya nauli vilivyoridhiwa
|
Daraja la kwanza la chini
(Low ordinary -lami
|
36.89
|
34.00
|
Daraja la kawaida chini
Lower
ordinary Bus
|
46.11
|
42.50
|
Darala la kawaida la juu
Upper
ordinary Buss
|
-
|
44.96
|
Daraja la kati
Semi-luxurry
Buss
|
53.22
|
44.96
|
No comments
Post a Comment