Zinazobamba

BENKI YA NMB YAZIDI WAJALI WATEJA WAKE,YAZINDUA KITU KIPYA,BWANA KIVARIA ASEMA NI HUDUMA POA SOMA HAPA KUJUA

Pichani ni Mkuu wa Kitego cha
Huduma Mbadala
wa Benki ya NMB
Bwana George Kivaria Akifafanua Jambo,
picha na Maktaba
KATIKA kuonesha inawajali wateja wake nchini Beki ya NMB imezindua Huduma yake bora ya kutoa pesa kwa haraka inayojulikana kama(NMB CHAP CHAP)Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
  Akitambulisha Huduma hiyo leo Jijini Dar es Salaam Mkuu wa Kitengo cha Huduma Mbadala wa Benki ya NMB nchini Bwana George Kivaria wakati wa Mkutano na waandishi wa Habari ambapo amesema Huduma ya hiyo wameianzisha mahususi kwa ajili ya kuwasogezea wateja wa Benki hiyo karibu na makazi yao ili iwape urahisi katika kutoa pesa.
      “NMB Chap chap ni akaunti kama akaunti nyingine isipukuwa inafunguliwa kama teknohama ya vifaa maalum kama simu na pos nje ya matawi yetu kwenye  maeneo ya wateja,vilevile inafunguliwa kwa mashart nafuu.”
     Bwana Kiviria ameongeza kuwa Huduma ya Benki chap chap itawasaidia wateja walioko mbali na Benki ya NMB ili wapate akaunti zakibenki na hatimaye waingie wote kwenye mfumo wa wigo rasmi wa kifedha ambapo anasema kwa kufanya hivyo anadai watajihakikishia ukuaji kwenye biashara kwenye Benki hiyo.
      Sanjari na Faida hizo Bwana Kirivia alizitaja taratibu za ufunguaji wa Akaunti katika Benki hiyo ni Mteja kuja pesa ya ths 100,00/yaani Tsh 5500/=garama za Kadi n ash 4500/=nyingine kama amana ya Akiba.
      Aidha, Bwana Kivira aliwataka wateja wa Benki NMB wakitaka kufungua Akauni za Chap chap wajitokeze na Pasipoti ya kusafiria,kadi ya kupiga kura,kadi ya kulipwa pension,utambulisho toka Afisa Mtendaji wa Kijiji,Leseni ya Udereva na kitambulisho cha Taifa..

       Pamoja na hayo amebainisha kuwa wateja wa Benki hiyo watanufaika kwa kuingia kwenye mfumo anao dai ni mzuri wa kibenki,kupata riba  na kufaidi gharama nafuu za kibenki pamoja na kutunza Fedha pahala salama na madhubuti.

No comments