NEC YAENDELEZA KIBURI CHAKE,SASA WAUNGANA NA PINDA KUFOSI KURA YA MAONI.SOMA HAPA KUJUA
TUME ya
Taifa ya Uchaguzi (NEC)imeendelea kung’ang’ania
zoezi la kura ya Maoni ya kupitisha Katiba iliyopendekezwa na Bunge maalum la
Katiba ifanyike tarehe 30 April mwaka huu,Anaandika KAROLI VINSENT.Endelea
nayo.
Kwa mujibu wa Tamko lilitolewa leo Jijini
Dar es Salaam na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na kusainiwa na Kaimu
mkurugenzi wa (NEC) Dk. Sist
Cariah linasema zoezi la upigaji wa kura ya maoni lipo pale pale ambayo ni
tarehe 30 April mwaka huu.
Na kwamba taarifa zilizoripotiwa na Vyombo
vya Habari pamoja na mitandao ya kijamii zikimnukuu Mwenyekiti wa tume ya Taifa
ya uchaguzi nchini (NEC) Jaji Mstaafu
Damian Lubuva kwamba tume
hiyo itaongeza mda wa kura ya maoni kutokana na kushindwa kuwaandikisha watu
nchi nzima kwa mwenzi mmoja uliobakia sio za kweli.
Akifafanua
taarifa hizo Dk Cariah anasema kwamba taarifa hizo hazina ukweli na kwamba tume
bado inahakika itamaliza zoezi la kuwaandisha wananchi kwenye Daftari la kupiga
kura kwa mda uliopangwa na kura ya maoni kufanyika tarehe ile ile ya 30 April
mwaka huu.
Amebainisha kuwa
kama wataitaji kuongeza mda watawaambia wananchi ila kwa sasa,Tume hiyo imeona
hakuna ulazima wa kufanya hivyo kutokana na kuwepo mda wa kutosha kuwaandikisha
wananchi kwenye Daftari la kupiga kura kwa mfumo mpya wa Biometric Voters Regislation,(BVR).
Kauli ya Tume
hiyo uchaguzi inakuja ikiwa ni siku chache kupita baada ya Waziri Mkuu Mizengo
Pinda kuutangazi ulimwengu kuwa kura ya maoni itafanyika tarehe 30 April mwaka
huu.
Kauli hizo za (NEC)
pamoja na Waziri mkuu Mizengo Pinda zimekuwa zikipingwa na wanasiasa pamoja
wanaharakati wakisema kura ya maoni haiwezi kufanyika kwa mda waliopanga
kutokana na tume hiyo ambayo sasa ipo katika mkoa wa Njombe ambapo wametumia
zaidi ya mwezi mmoja sasa kwahiyo kwa mwezi mmoja uliobaki hawawezi kukamilisha
kuwaandikisha watu wa mikoa zaidi ya 22
kwa mwezi mmoja.
Kwa Mujibu wa Mtoa Taarifa wetu kutoka Kwenye Tume ya Taifa ya Uchaguzi
NEC ameumbia Mtandao huu kwa sasa kinachosema na viongozi wa tume hiyo
pamoja na viongozi wa Serikali kulazimisha kura ya maoni kufayika kwa mda huo
ni kujidanganya.
“Sikufichi hapa tunafosiwa na Rais
tufanye tuwezavyo tuwe tumemaliza Mwezi wa nne wakati uwezekano ni
mdogo,kwasababu Daftari la kudumu haliwezi kukamilika kwa mda huo.yaani kama
vifaa vikiwepo vyote vinavyoitajika basi Daftari linaweza kukamilika
mwishoni mwa mwezi juni,yaani hapa hata wafanyaje hiyo kura haipigiki
mwezi wanne”ameeleza.
Taarifa za Kumanika ambazo mtandao huu
umedokezwa zinazidi sema hadi kufikia jana,NEC ilikuwa na mashine 250 tu za
kuendesha zoezi hilo,huku matatizo mengi yakiwa yamejitokeza katika
uandikishaji wake unaoendelea Mji mdogo wa Makambako Mkoani Njombe.
Licha ya vifaa hivyo kuwa vichache
tayari nchi jirani ikiwemo Kenya wameigomea Serikali nchini ambayo ilikuwa
inataka kuazimwa mashine hizo za (BVR)
Mtoa taarifa huyo
alizidi kuambia mtandao huu kwamba Shehena ya Mwisho ya Vifaa inatarajiwa
kuwasili nchini katikaki ya mwezi Juni mwaka huu.
Kwa mujibu la Andishi laNEC
lilisema tume hiyo inahitaji mashine 15,000,Lakini serikali imeridhia
kununuliwa mashine 8000,jambo la kushangaza NEC imepewa Mashine 250 tu
kuendesha zoezi hilo ,Mradi huo ambao unagharimu zaidi ya Bilioni 293 za
kitanzania.
Kulazimishwa huko na Rais Kikwete kwa tume ya uchaguzi ili kuharakisha
uandikishaji wa wapiga kura kunakuja huku ikiwa tayari vyama vikuu vya Upinzani
nchini kupitia umoja wao,kutaka kura hiyo ya Maoni isitishwe kwa kuwa
haitoweza kufanyika kwa ufanisi na kwamba badala yake serikali iwekeze nguvu
zake katika kufanikisha uchaguzi mkuu utakofanyika baadae mwa mwaka huu.
Mbali na Vifaa
vya uandikishaji huo,kumekuwa na mapungufu mengi yamejitokeza ambao watendaji
wa NEC wamethibitisha kutokea.
“Waandikishaji
wanababaika,watu wengi,wanapanga foleni kutwa zima,halafu mara waambiwa
kamera,halafu mara wanaambiwa mashine mbovu tena wanaambiwa kamera imegoma”
“La ajabu zaidi
tumeshuhudia mashine imeshindwa kusoma alama za vidole wenye usugu” ameeleza
mtoa taarifa wetu wa NEC aliyoko Makambako
No comments
Post a Comment