Zinazobamba

KAMPENI YA KUTAMBUA NGUVU ZA MWANAMKE KATIKA UKOMBOZI WA TAIFA LA TANZANIA YAZINDULIWA




Ile kampeni  ya kutambua na kuenzi mchango na nguvu za wanawake katika historia ya taifa la Tanzania imezinduliwa limezinduliwa mapema hii eo jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa sanaa za jukwaani, Makumbusho ya Taifa.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo,  Kaimu mkurugenzi mkuu wa Makumbusho ya Taifa Bi. Adelaide Sellema , amesema “katika historia ya taifa, ni mara ya kwanza kufanya kazi maalum ya kutambua historia ya wanawake katika jamii kwa malengo ya kuweka kumbukumbu sahihi kwa maendeleo ya historia ya Tanzania kwa vizazi na vizazi”.
Amesema, kwenye siasa na harakati za ukombozi wa Tanzania, yanatajwa majina ya Mwani Theresa Ntare- aliyekuwa chifu wa Kasulu aliyesimamia vyema msimamo wa Baraza la Machifu mwaka 1958 na kuunga mkono juhudi za TANU katika kudai uhuru.“Bibi Titi Mohamedi ambaye alikuwa kiongozi wa TANU- Women Wing aliweza kutengeneza historia ambayo sio rahisi kufikiwa au kuvujwa na kiongozi wa vyama vya siasa katika mazingira ya sasa,” lakini bado wamekuwa hawapewi kipaumbele kinachostahili
Ameongeza kuwa yupo pia Sophia Mustapha (mwenye asili ya Ki- asia) ambaye pamoja na sera za kibaguzi, zilizokuwa zimewekwa na wakoloni za kuwabagua raia kwa misingi ya rangi, aliamua kuunga mkono juhudi za TANU na alishiriki siasa na hatimaye kuingia katika baraza la kutunga sheria.
Aidha, kwa upande wake  Mkurugenzi mtendaji wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) Lilian Liundi  , amesema dhima ya kampeni hiyo ni “Uthubutu wa mwanamke na miaka 54 ya maendeleo ya Tanzania” huku kaulimbiu ikiwa ni “Mwanamke, Historia yetu, fahari Yetu”.
Katika kampeni hiyo ambayo imezinduliwa inatarajiwa kukusanya Taarifa  zitakazotumika kuwaenzi wanawake kama sehemu ya kuhamasisha vizazi vya sasa na vijanvyo umuhimu wa ushiriki wa wanawake katika maendeleo endelevu.
“Kuendeleza mijadala kuhusu michango na ushiriki wa wanawake na kudai uelekezaji wa rasilimali kutoka kwa wadau mbalimbali katika kuendeleza ushiriki wanawake na kuwaenzi,” amesema Liundi.
Kampeni hiyo itachukua muda wa miaka mitatu. Inatarajiwa kuhusisha wadau mbalimbali wakiwemo TGNP Mtandao, Makumbusho ya Taifa, Women Research Development Project, Women Fund Tanzania (WFT), Soma na shule ya uandishi wa habari ya RAIDA
Kwa mujibu wa wadau ambao wamefika katika sherehe za uzinduzi huo wamekiri na kusema kuwa mradi huo ni muhimu sana katika kufanya vizazi vyetu kujua mashujaa ambao wamefanya kazi kubwa katika taifa hili la Tanzania.

No comments