Zinazobamba

JIMBO LA UKONGA LAZIDI KUTEKWA NA CCM,BODABODA WAAPA KUFA NAE MBUNGE ALIYOPO,SOMA HAPA KUJUA


CHAMA Cha Mapinduzi CCM,kinazidi kujihakikishia kushinda nafasi ya Ubunge kwenye Jimbo la Ukonga lililopo Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam kwenye uchaguzi Mkuu utakaofanyika mwishoni mwa Mwaka huu.Anaandika KAROLI VINSENT,Endelea nayo.
        Jimbo  hilo la Ukonga ambalo linaongozwa na Mbunge mwanamama Eugean Mwaiposa ,kwa sasa ni wazi dalili zinaonekana atazidi kupeta kwenye Uchaguzi huo,baada ya Vijana Madereva maarufu Bodaboda wa Jimbo hilo kuibuka na kuaapa kumpigania ashinde tena kwenye kiti hicho.
     Kiapo hicho Kimtangazwa na Bodaboda hao mda huu Jijini Dar Es Salaam wakati wa kufunga Semina iliyoandaliwa na Mbunge huyo kwa ajili Bodaboda hao, yenye lengo ya kuwapa mafunzo ili kujikinga na Ajali mbalimbali ambazo zimekuwa zikiwakumba.
      Ambapo wakitoa kiapo hicho kwa pamoja Bodaboda zaidi ya Mia tano kutoka Jimbo la Ukonga wamesema hawaoni sababu ya kutomuunga mkono mwanamama huyo kwani amekuwa ni mtu pekee anayewajali wananchi wenye lika zote  hususani wao bodaboda.
       Aidha, Bodaboda hao wamesema kwa sasa watahakikisha wanawashawishi Bodaboda wengine pamoja na wananchi wa Jimbo la Ukonga kumchagua Mbunge huyo kwa kuwa ni Kimbilio lao.
     Naye Mbunge Mwenyewe Mwaiposa amewashukuru sana bodabosa hao kwa kujua uwezo wake wa kazi na akawataka kuonyesha ushikamano katika masuala ya Maendeleo ya Jimbo hilo kwa kipindi kifupi kilichobakia.
Kuibuka kwa Bodaboda hao kunampa wakati Mgumu Meya wa wa Wilaya ya Ilala Bwana Jerry Slaa ambae inadaiwa na marafiki zake wa karibu ambao wanasema Meya huyo anainyemelea nafasi hiyo.

Jerry Slaa ambaye ni Diwani wa kata ya Majani ya Chai iliyopo katika Jimbo hilo na pia ni Mjumbe wa Kamati kuu ya Chama cha mapinduzi cc, amekuwa akiandaa mipango inayoitwa ni ya ‘Kimyakimya”ya kumrithi mwanamama huyo mwenyeji wa Mkoa wa Mbeya. 

Hakuna maoni