HABARI KUBWA LEO.NI VITA MAASKOFU NA MASHEHE,WAISLAM WATOA MASHARTI MAZITO KWA KIKWETE,WAIRUSHIA KOMBORA BWAKWATA,SOMA HAPA KUJUA
| Pich ani niNaibu Katibu Mkuu Taasisi ya Kiislam nchini Sheikh Rajab Katimba Akuzungumza na wanahabali leo |
NA KAROLI
VINSENT
TAASISI ya
dini ya Kiislam imeita serikali kuwakamata maaskofu na wachungaji ambao wanadai
wametoa matamko ya kichochezi na endapo serikali ikikaidi kuwakamata, basi
jumuiya hiyo itawahamaisha waamini wa dini ya kiislam popote walipo kuipigia
kura ya Hapana Katiba inayopendekezwa na Bunge Maalum la Katiba.
Kauli ya taasisi hiyo yenye misimamo
mikali inatokana na Tamko walilotoa muunganiko wa jumuiya ya Kikristo,ikiwemo
Baraza la Maaskofu katoliki (TEC),Jumuiya ya Kikristo Tanzania(CCT),Baraza la
Makanisa la kipentekoste(CPCT)ambao wote kwa pamoja waliiwataka waunini wa dini ya
kikristo nchini kuipigia kura ya hapana katiba,kutokana na serikali kuruhusu mahakama ya Kadhi kisheria.
Akitoa tamko la Taasisi ya Dini ya
Kiislam ambalo ni muunganiko wa taasisi
ya dini hiyo zaidi ya 11 hapa nchini ,Naibu Katibu Mkuu Taasisi hiyo Sheikh
Rajab Katimba wakati wa Mkutano na Vyombo mbalimbali vya Habari leo Jijini Dar
es Salaam-
Ambapo
Sheikh Katimba huku akiongea kwa uchungu ameitaka serikali iwachukulie hatua
maaskofu hao kwa madai ya kufanya uchuchezi na kuvunja katiba ya nchi.
“Serikali iwachukulie hatua za kisheri
maaskofu na wachungaji kwa kutoa matamko yakichochezi yaliyokusudia kuumiza
hisia ya kidini kwa waislam kinyume cha sheria ya kanuni ya Adhabu sura ya 16
ikiwemo kuwakamata,kuwafikisha mahakamani na kuzuia dhamana kama inavyofanya
kwa masheikh pindi wanapotoa kauli zinazopingana na mtazamo wa serikali lasivyo
hatutaipigia kura katika iliyopendekezwa”amesema Seikh Katimba.
Sheikh Katimba ameongeza kuwa Serikali
imetoa rushwa kwa Waislam na kwa kundi maalum kwa kukubali sheria itakayounda
mahakama ya Kadhi ili kuipitisha katiba iliyopendekezwa ambapo amesema ni
kuidhalilisha dini ya mwenyezi mungu ikiwemo kuwadhalilisha waislam na ni
kuumiza hisia ya waislam na kuhatarisha amani na utangamano.
Amebainisha kuwa Serikali iendelee na
Mchakato wa uundwaji mahakama ya kadhi kwa kufuata maoni yaliyotolewa mbele ya
kamati ya sheria na utawala wa bunge kwa kuzingatia mambo muhimu.
Aliyataja mambo muhimu hayo ikiwemo ni
serikali iache njama anazodai na hila za kuigeuza mahakama ya Kadhi
inayohitajika kuwa miliki ya taasisi ya BAKWATA na MUFTI wa BAKWATA.
“Endapo serikali itaendelea na
kuwasilisha muswaada wa Mahakama ya Kadhi unaoipa mamlaka Bakwata kuunda,kusimamia,kuteua
makadhi nakadhalika kinyume na maoni ya Waislam wengi itakuwa imethibitisha
kuwa serikali haikuwa na nia ya kweli ya kuunda na kuanzisha mahakama ya Kadhi”ameendelea
kusema Sheikh Katimba
Aidha,Sheikh katimba amesema serikali
igharamie mahakama hiyo kama ambavyo anadai serikali hivi sasa inavyogharimia
uendeshaji wa mashauri yaliyopo kwenye mahakama za kawaida yanayohusu sheria za
kiislam ambayo mara nyingi yanaamuliwa kwa makosa.
“Na pia
igharamiwe na serikali ambavyo serikali hii inavyogaramia huduma za makanisa chini
ya mkataba maarufu memoradum of understanding (MOU)mkataba ambao haukuwahusisha wala kutaka ridhaa ya
waislam”ameongeza kusema
No comments
Post a Comment