Zinazobamba

HABARI KUBWA-CUF YAMUUMBUA ZITTO,YASEMA AMEJIUA KISIASA MWENYEWE SOMA HAPA KUJUA


CHAMA cha Wananchi CUF ni kama kimemshukia Aliyewai pata kuwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe (pichani) kwa kusema ni mwanasiasa jeuri ambaye hana maana ana anafaa kupuuzwa.Anaandika KAROLI VINSENT.endelea nayo.
             Zitto Kabwe ambaye amejiuzulu Ubunge mwishoni mwa wiki iliyopita ili kuepuka aibu ya kufukuzwa Ubunge na Spika wa Bunge Anna Makinda baada ya Chama cha Demokrasia na maendeleo Chadema kumfukuza uanachama wa chama hicho baada kutupiliwa mbali kesi yake mahakamani aliyoifungua-
Kupinga maamuzi ya kamati kuu ya Chadema yaliyomfukuza kwenye chama hicho kutokana na kudaiwa kwake kuandaa mipango ya kuwapindua viongozi wa wakuu wa chama hicho.
      Kabwe ambapo siku moja baada ya kujiuzulu amejiunga na chama cha ACT-Tanzania ambacho inadaiwa alikuwa nakimiliki 'kinyemela"tangu mwanzo
         Akizungumza na Mwandishi wa mtandao huu Naibu Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CUF Abdual Kambaya mda huu kwenye makao mkuu ya chama hicho yaliyopo Jijini Dar es Salaam ambapo pamoja na mambo mengine alizungumzia hali ya kisiasa ya Zitto Kabwe  kwa kumtabilia mwanasiasa huyo kupotea kwenye medani ya kisiasa nchini.
           “Mimi namfahamu zitto kuwa ni mtu makini sana tena mwenye maono makubwa,lakini kitendo chake alichokifanya cha kuhamia ACT ni wazi amejiharibia kabisa kwani hata iko chama alichokwenda hakina viongozi wenye uwezo wa kujenga chama,kwa mfano Katibu wa ACT mwigamba ni mtu ambaye amezoea siasa za hovyo na sidhani kama atafika mbali na chama hicho”amesema Kambaya.
            Kambaya ameongea kuwa kitendo cha zitto kabwe kuhama chadema kilionekana tangu mwanzo kwani amedai mwanasiasa huyo ni kiburi na asiyeweza kushaurika.
         “ Kama mtu makini sana ukimuangalia zitto utamgundua ni mtu mwenye tabia ya kujiona na hiyo imetokana na yeye kujikuta yuko juu baada ya kulewa sifa kutoka kwa wananchi na sababu hiyo ndio inamuharibia sana na hawezi fika mbali “

          “Na atafuata nyayo za wanasiasa kama wakina Mrema yuko wapi leo na alikuwa anawafuasi wengi kuriko yeye hebu jiulizeni leo  vipi”ameongeza Kambaya.
    Katika hatua nyingine Chama cha CUF kimeitaka serikali kuacha tabia ya kung’ang’ania kura ya maoni ya kupitisha katiba iliyopendekezwa na Bunge maalum la Katiba kufanyika tarehe 30 April mwaka huu, kwa kusema hakuna uwezekano wa kufanyika-

     kwa tarehe kwa madai tume ya Uchaguzi nchini (NEC) imeshindwa katika zoezi lake la kuwaandikisha wananchi kwenye Daftari la kudumu la wapiga kura kwa mfumo mpya wa (BVR)
       Akizungumza kwa niaba ya chama cha CUF, Mkurugenzi huyo wa Mawasiliano wa Chama hicho Abdual Kambaya amesema kwa sasa ni wazi serikali inajidanganya kufosi kura ya maoni kufanyika tarehe hiyo .

No comments