Zinazobamba

HABARI NJEMA-PATO LA TAIFA LAKUA KWA KASI,TAKWIMU YASEMA HALI NI NJEMA SOMA HAPA KUJUA

Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Bw. Morrice Oyuke akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Picha na Maktaba



PATO la Taifa limeongezeka kwa kasi ya asilimia 6.8 katika   kipindi cha robo ya tatu mwaka 2014 ikilinganishwa na kasi ya asilimia 7.4 katika kipindi kama hicho cha mwaka 2013.Anaripoti KAROLI VINSENT,Endelea nayo.
            Hayo yametangazwa mda huu jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi uchumi na Fedha wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Bwana Morrice Oyuke Wakati wa Mkutano na waandishi wa Habari ambapo amesema Matokeo ya Takwimu za pato la Taifa kwa robo mwaka kwa bei ya miaka inayohusika yameonyesha -
        kuwa thamani la pato la taifa katika kipindi cha robo tatu ya mwaka 2014 ilikuwa trilioni 21.2 kwa mwaka 2014 ukulinganishwa na 19.8 trilioni kwa mwaka 2013.
           Bwana Oyuke ameongeza kuwa pato la taifa kwa bei za mwaka 2007 katika kipindi cha robo mwaka ya tatu linaonyesha kuwa jumla ya thamani ya 10.7 trilioni  mwaka 2014 ikilinganishwa na 10.1 trilion kwa mwaka 2013 katika kipindi hicho.
              Alibainishwa kuwa ukuaji wa pato hilo umetokana na shughuli za kiuchumi ikiwemo-
            Ukuaji wa Sekta ya Kilimo na Mifugo ambapo zilikuwa kwa asilimia 3.1 katika kipindi cha robo mwaka ya tatu ya mwaka 2014 ukulinganisha na kasi ya ukuaji wa asilimia 3.4 kwa mwaka 2013.
             Mbali na hizo alizitaja shughuli zengine ni za uchumi za viwanda na ujenzi ,shughuli za uchimbaji wa madini,mawe,shughuli za uzalishaji nisharti ya umme,uzalishaji wa viwandani ambazo zote kwa pamoja zimekuwa kwa kasi kubwa ukilinganisha na mwaka 2013

Hakuna maoni