Zinazobamba

HABARI KUBWA LEO-DILI LA KATIBA MPYA LAVUJA,NI LA RUGE WA CLAUDS RADIO NA MAKONDA SOMA HAPA KUJUA



http://mtanzania.co.tz/wp-content/uploads/2014/07/Jakaya-Kikwete1.jpg
RAIS KIKWETE




IKULU ya Rais Jakaya Kikwete  bado inaendelea kulazimisha katiba iliyopendekezwa  na Bunge  maalum la Katiba kupigiwa kura ya ndio na wananchi ,huku ikiwa kinyume na sheria ya kura za maoni.Anaripoti KAROLI VINSENT endelea nayo .
     Habari za kuaminika ambazo mtandao huu umezipata zinasema kwa sasa kumekuwa na mpango unaoandaliwa na Ruge Mutahaba na kusukwa kwa karibu paul Makonda,Katibu wa uhamisishaji wa Umoja wa vijana wa Chama cha Mapinduzi CCM,mpango huo wenye kugharimu Sh.Milioni 588.4 za kitanzania.
        Mpango huo unaratibiwa na kinachoitwa  “Kamati ya kusimamia utangazaji  wa katiba iliyopendekezwa” iko chini yaOfisi ya Ikulu.
          Ruge ambaye ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Clouds media ambayo inamiliki Radio ya Clouds Fm,Clouds Tv ambapo amependekeza fedha hizo zitumike kwa ajili ya kugharamia vyombo vya Habari,wasanii wa kizazi kipya,mchiriku na muziki wa Taarabu.
           Kwa mujibu wa sheria ya kura ya maoni unaiumbua Ikulu ya Rais Kikwete baada ya sheria hiyo kusomeka kwamba kura ya maoni ,Serikali haipaswi  kuegemea upande wowote katika pande mbili –inayounga mkono katiba inayopendekezwa au inayopingwa.
         Kuibuka kwa mipango hiyo ambayo serikali imekuwa na mradi wake huu,kumekuja takribani miezi miwili baada ya kuvuja mkakati wa kwanza uliokuwa unaratibiwa na ikulu na ulikuwa unatafuta kura ya "ndio" kwa Katiba iliyopendekezwa.
         Mkakati huo uliibuliwa na Katibu mkuu wa Chama cha Maendelea Chadema Dk Wilbroad Slaa ambapo Slaa aliwaambia waandishi Habari kuwa Mkakati huo aliunasa ulikuwa unatoka kwa Katibu Mkuu wa Rais kwenda kwa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Salva Rweimamu.
       Katika Andishi hilo Mkurugenzi huyo wa mawasiliano ya Rais alishauri bajeti ya Sh.Bilioni 2.5 .mkakati huo ulikuwa unapangwa kuwalaghai wananchi kuipigia kura ya Ndio katiba iliyopendekezwa na bunge Maalum la Katiba.
       Waraka huo ambao Salva,alikiri kuwaandaa na kusema kikao cha awali kilikuwa kinafanyika na kuwashirikisha wahariri wa Vyombo vya Habari nchi.
          Ambao ni Assah Mwambene Mkurugenzi wa Maelezo,Saidi Yakubu afisa mwandamizi kutoka ofisi ya Bunge,Gabriel Nderumaki Mhariri Mtendaji wa Magazeti Ya Serikali,Joseph Kulagwa mhariri mtendaji wa Gazeti la Chama cha Mapinduzi CCM la Uhuru na Mzalendo na Angel Akilimali naye ni Mkurugenziwa Radio Uhuru.
          Kwa Mujibu wa Mpango wa Ruge Mtahaba  umewataja wasanii mbalimbali kutumika,wanaoelezwa kutumika kulaghai wananchi ili kupigia kura ya ndio ni Khadija Kopa,mzee yuseph,Isha Mashauzi,Hussen Mohamed (Hammer q),Barnaba Elias,EsterLinah Sanga,Mwasiti Almas,Mwasiti Almas,Mataluma,Madee,Godzilla,Yamoto Band,Omy Dimpoz,Chege na Temba,Vanesa Mdee na Hamis Mwijuma (mwana FA).

Hakuna maoni