Zinazobamba

HABARI ILIYOTIKISA JIJI-WAZIRI MWAKYEMBE NDIYE ANAYEKUMBATIA MAFISADI NDANI YA BANDARI,AMLEA MKURUGENZI



Na Karoli Vinsent
      SIKU moja kupita baada ya Kamati ya Kudumu ya Bunge inayoshughulika na Hesabu za Mashirika ya Umma (PAC) kufichua matumizi mabovu ya kifisadi ya zaidi  sh bilioni 20 zilizotumika katika mkutano wa wafanyakazi, matangazo na safari za ndani na nje za vigogo kinyume na taratibu ndani ya  Mamlaka ya Bandari nchini,
       Naye waziri wa Uchukuzi Dk Harison Mwakyembe Ameingia kwenye Kasfa Nzito ,kutokana na Kitendo chake cha kushindwa kumchukulia hatua,
pichani niKaimu mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA),Mzee Maden Kipande
        Kaimu mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA),Mzee Maden Kipande,ambaye ameguza Mamlaka hiyo kuwa Genge la Ufisadi na kupelekea mabilioni ya fedha kupotea.

     Dk Mwakyembe,ambaye anasifika kwa Wananchi kutokana              Uchapakazi wake na kutokuwa na Nidhamu ya Uwoga asiyemwogopa mtu yeyote ,ambae atakuwa anavunja Sheria za Nchi, alikuwa anamwajibisha.
Lakini,mambo yamebadilika kwa Waziri hiyo,ambapo sasa ameonekana ameshindwa kumchukulia hatua,Kaimu mkurugenzi wa Mamlaka ya Bandari Kipande,kutokana na Vitendo vyake vya kifisadi huku vyombo vya Habari pamoja na kamati za bunge kufichua ufisadi anaofanya.
Pichani ni WAZIRI wa Uchukuzi Dk Harison Mwakyembe

       Kwa Mujibu wa vyanzo  vya kuaminika ambavyo mtandao huu umezipata kutoka katika Mamlaka hiyo ambayo ni kitovu cha Maendeleo ya Nchi yetu  amezipata ,zinasema mkurugenzi huyo amekuwa akiwasimamisha wafanyakazi kinyume na Taratibu na sheria.
       Chanzo hicho kinasema mkurugenzi huyo,amekuwa akiwasimamisha watu tu pasipo kuwa na kosa lolote kwa mfano miezi  iliyopita ameanzisha Mpango wa kumngoa Meneja wa Bandari ya Tanga,Hassani Kyomile eti akisema Meneja huyo amekuwa akivujisha siri kwenye Gazeti moja la wiki  akidai    Mhariri wa Gazeti moja la wiki ambalo limekuwa likifichua habari zake kwa madai mhariri huyo  ni Mhaya ,na meneja huyo pia nimhaya  anavujisha siri kwenye Gazeti hilo,
   Ambapo kipande anaona kumfukuza meneja huyo kutarahisisha mipango yake ya kifisadi pasipo kuvuja.
        Chanzo hicho kilizidi kusema  Kipande amekuwa akijivunia kwa Wanyakazi wake kwamba anaweza kufanya lolote na hakuna wakumzuia,na amesimamisha watu kazi zaidi ya miaka miwili huku  wakiwa wakipokea mishahara pamoja na malupulupu  wakiwa nyumbani bila hata ya kufanya kazi.
    Chanzo hicho kiliwataja wafanya kazi hao,miongoni mwao ni Mama Muhindi,ambaye alikuwa Mkurugenzi wa Masoko TPA,ambaye alisimamishwa kazi na Kipande kwa Madai alikuwa anavujisha siri(madudu)za TPA kuhusu  kwenye vyombo vya        Habari,licha ya mkurugenzi kipande alishindwa kutokea wala kukanusha kwenye vyombo vya Habari juu ya Ufisadi huo ,
        Tuhuma,zinginene zinazozidi kumkabili kipande kuhatarisha  usalama wa Bandarini kwa kutokuna na kutokuwepo na Kamera CCTV pamoja na mita za kupima mafuta yanayoingia nchini kutokafanya kazi kwa miaka mitatu sasa.
      Jambo la kushangaza Mama huyo Muhindi,alisimaishwa kazi tangu agosti 2013 na kipande,lakini  hajahojiwa wala kurudishwa kazini ,huku akizidi kuendelea kuchukua mshahara na Marupumarupu mengi bila kufanya kazi hadi sasa wala hajahojiwa na mamlaka yeyote.
       Chanzo,hicho kilizidi kutaja orodha ya Wafanyakazi  walionewa na Kipande ambae ni Mfanyakazi  mwingine ndugu Msemo,aliyekuwa Afisa Ununuzi,naye alisimamishwa kazi tangu agosti2013 kwa tuhuma zisizokuwa za Ukweli wowote, lakini mpaka sasa naye anaendelea kuchukua mshahara pamoja na marupurupu yote pasipo kufanya kazi.
        Waliosimamishwa na kipande kwa tuhuma hewa
Hery Arika,aliyekuwa Men eja Biashara wa Bandari ya Dar es Salaam,alihamishiwa makao makuu na kuambiwa kuripoti idara ya utawala tangu April 2013 hadi leo hii,Analipwa mishahara na marupurupu yake bila kufanya kazi kwa mwaka mmoja sasa,kwa madai ya Kipande hamtaki.
    Ajira za Upendeleo,
Kama kuna mgogoro unaofuka Moshi Ndani ya Bandari basi ni huu unaotokana na  Ajira za Mhandisi Alois Matei,ambaye ni Naibu Mkurugenzi mkuu(Maendeleo ya Miundombinu)na mhandisi William Shilla,ambaye ni mkurugezni wa Uhandisi.Taharifa zilizopo zinasema kuwa Wahandisi hawa wawili waliajiriwa  na Kipande kupitia Mlango wa Nyuma ,pasipo kufuata  taratibu za sheria.
      Huu ni Mwenderezo wa Unyama unaofanywa na Kipande ndani ya Bandari pasipo kuchukuliwa Hatua yeyote kutoka kwenye Taasisi za Kupambana na Rushwa TAKUKURU,wala Wizara husika ya Uchukuzi ambao,mamlaka hiyo iko chini yake.
      Huku,Kipande akinijinadi kwenye mkutano na Uongozi wa mamlaka hiyo,akisema mtu yeyote atakaye pingana nae anamng’oa kwani yeye na mamlaka  ya Bandari hawapati hasara yeyote bali serikali ndio inapata hasara,na kama yuko mtu yeyete atakaye pingana naye(Kipande )basi atamfukuza Kazi.
      Duru, hizo zinasema mzee Kipande amekuwa akifanya Vitendo hivyo vya Kifisadi huku akijinadi Hakuna mtu wa kumng”oa nafasi hiyo kwa Madai,eti anajuana Kigogo mmoja aliyoko  Ikulu ya Rais Jakaya Kikwete,ambae amekuwa karibu na Kipande.Ndio maana Amekuwa akifanya Vitendo hivyo akijua hakuna mtu wakumchukulia Hatua zozote.
Chanzo ni Gazeti la Jamhuli


Hakuna maoni