KILWA ENERGY NA MALIPO YA UKANDAMIZAJI KWA WANANCHI, NI FIDIA YA KUPISHA UJENZI WA NJIA YA UMEME WA KILOVOLT 220 TOKA SOMANGA HADI KINYEREZI, WAITAKA SELIKARI KUINGILIA KATI ZOEZI HILO..
Dar es Saalam.
Wananchi wa Mji Mpya Majohe, Guluka Kwalala na Ulongoni katika Manispaa ya Ilala wameiomba Serikali kuingilia kati na kumwamuru mwekezaji wa ujenzi wa njia ya umeme wa kilovoti 220 kutoka Somanga Mtama mpaka Kinyerezi, Kilwa Enegy kuwalipa gharama zinazoendana na hali ya maisha ya sasa.
Wananchi wa Mji Mpya Majohe, Guluka Kwalala na Ulongoni katika Manispaa ya Ilala wameiomba Serikali kuingilia kati na kumwamuru mwekezaji wa ujenzi wa njia ya umeme wa kilovoti 220 kutoka Somanga Mtama mpaka Kinyerezi, Kilwa Enegy kuwalipa gharama zinazoendana na hali ya maisha ya sasa.
Ombi hilo walilitoa jana walipokuwa wakijadili
kuhusu dodoso la uhakiki wa mali zao na malipo, walilopewa lilivyokuwa
na upungufu, mapunjo ya mali zao hasa thamani za nyumba kuwa kidogo
tofauti na gharama za ujenzi na ununuzi wa kiwanja walizotumia.
Utathmini wa mali na nyumba za wananchi unadaiwa
kufanywa na kampuni binafsi iliyofahamika kwa jina la Joransa, ambapo
tathmini katika maeneo hayo ilifanyika mwaka 2011 na kutolewa ahadi kuwa
malipo ya fidia yangeanza kulipwa baada ya miezi mitatu .
.Baruani Kanoze akilalamikia kulipwa fedha
kidogo tofauti na thamani ya mali zake, alisema mwekezaji huyo awali
aliwahi kusema kuwa atawalipa kwa kiwango kinachoendana na gharama za
maisha zilivyo kwa wakati husika jambo ambalo limewashangaza sana. hasa
kulingana na kiwango cha malipo kilichotolewa.
‘Ni jambo ambalo haliingii akilini baada ya
kuangalia karatasi za tathmini na kukuta gharama zilivyowekwa za viwanja
na kupangisha nyumba, kiwanja umewekewa Sh1 milioni na gharama ya
kupanga nyumba eti Sh20,000 kwa mwezi, sijui unakwenda kupanga wapi
nyumba’ alisema mkazi wa Guluka Kwalala ambaye hakutaka kutajwa
gazetini.
Alisema yeye anamiliki nyumba ya vyumba vitano,
yenye umeme, choo bora pamoja na kisima cha maji alivyovijenga kwa
zaidi ya Sh40 milioni, kwenye dodoso la uhakiki wa mali anaambiwa
thamani ya nyumba yake ni Sh6 milioni.
Aidha, walishauri kuliko Serikali kujiingiza
katika maafa kwa kukubali mradi huo utekelezwe wakati wananchi
hawajaridhika na fidia ao, ni vyema ikafanyika tathmini nyingine ambayo
itakuwa ya haki .
Hata hivyo, uongozi wa Kilwa Energy ulipotafutwa kufafanua malipo hayo ya wananchi, simu zao hazikuweza kupatikana.
No comments
Post a Comment