Zinazobamba

BABALEVO AJIUNGA BROTHERS ACADEMY KUJIENDELEZA KIELIMU.


Na Mussa Augustine.

Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini Revocatus Chipandu( Baba levo )amejiunga na shule ya Brothers Academy kwa ajili ya kujiendeleza kielimu.

Akizungumzia na Waandishi wa habari mapema leo Februari 11,2026 Mbunge huyo amesema kuwa dunia ya sasa hata kama una kipaji cha kufanya lakini unaweza kukwama kutokana na kigezo cha Elimu hatua ambayo imemfanya ajiunge na shule ya Brothers Academy ili aweze kupata Elimu. 

"Nimejiunga na Brothers Academy kutokana na kwamba wana programu ya VIP ambayo unaweza kuhudumiwa mahali popote,mimi ni Mbunge,nina kazi nyingi za kuwahudumia Wananchi wa Kigoma Mjini,lakini pia natakiwa kusoma, hivyo hii shule(Brothers Academy)ina programu za kufundisha watu wa VIP kama mimi" amesema Baba Levo.

Aidha ameongeza kuwa Shule ya Brother's Academy inatoa Elimu kuanzia darasa la saba,kidato cha kwanza hadi kidato cha sita kwa muda wa miaka 3,hivyo amewaomba,watu maarufu na Wananchi wote wanaotamani kujiendeleza kimasomo wajiunge na Brothers Academy ili kutimiza ndoto zao.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Brothers Academy Bw.Robert Rwezaula amemshukuru baba levo kwa kijiunga na shule hiyo huku akisisitiza kuwa atapata Elimu iliyo bora kutokana na shule hiyo kuwa na walimu wabobevu.

"Mh.hujakosea kijiunga nasi,na tumekua na bahati kubwa yakua na mtu wa kwanza mashuhuri kwenye shule yetu,ukifanikiwa utakua ni balozi wetu na tunaamini tutapata watu wengi watakaojiunga na shule yetu" amesema Mwalimu Rwezaula.

Aidha amesema kuwa Shule ya Brother's Academy inatoa Elimu kwa  gharama nafuu ya kiasi cha shilingi 2500,000 kwa mwaka na hulipwa kwa awamu nne yaani Januari,Aprili,Julai na Septemba.


#brother'sacademy.

No comments