WAUMINI WA BCIC MAJIMEUPE WATOA MSAADA HOSPITALI YA MAJI MATITU KUELEKEA MAADHIMISHO YA MIAKA 15.
Na Mussa Augustine.
Waumini wa Kanisa la BCIC Majimeupe Kanda ya Dar es salaam wametoa zawadi ya vifaa mbalimbali ikiwemo viti,sabuni,taulo za kike,mifagio nakufanya usafi katika hospitali ya Maji Matitu kwa ajili ya kuwasaidia wakina mama wajawazito wenye mahitaji mbalimbali.
Akizungumza leo Juni 8,2024 wakati wa kukabidhi vifaa
hivyo Askofu Mkuu msaidizi wa BCIC Majimeupe kanda hiyo Askofu Michael Petter
Imani amesema kuwa hatua hiyo inatokana na kuelekea maadhimisho ya miaka kumi
na tano ya kanisa hilo inayotarajiwa kufanyika siku ya jumapili ya tarehe 9 Juni
,2024.
Askofu Imani ambaye pia ni Askofu Mkuu wa Kanda ya Dar es
salaamu na Pwani pamoja na Mchungaji kiongozi wa kanisa hilo, amesema kuwa BCIC
Majimeupe limefanya mambo mengi yakujivunia ndani ya miaka kumi na tano ya
uinjilishaji ikiwemo kubadilisha tabia ovu za baadhi ya watu nakuwafanya
waachane na matendo mabaya kama vile ulevi,uasherati pamoja na wizi.
“BCIC Majimeupe kesho tunaadhimisha miaka kumi na tano tangu
kuanzishwa kwa kanisa hili hapa mbagala majimatitu mwaka 2009,hivyo leo
tumekuja hapa hospitalini ili kutoa mchango wetu mdogo wa vifaa mbalimbali
ikiwemo sabuni,viti,taulo za kike na fedha kidogo ikiwa ni sehemu ya
kuwakumbuka wagonjwa na kuwafariji “amesema Askofu Imani.
Nakuongeza kuwa”Kulikua na mambo mengi mabaya hapa maji
matitu yakiwemo masuala ya ushirikina hadi watu walikua wanashindwa hata
kujenga nyumba na barabara lakini tangu BCIC Majimeupe kuanzishwa hali imebadirika sana,kwa sasa tuna waumini takribani 2000 na wananchi wengi wanajitokeza kumpokea yesu
kristo kuwa mwokozi wa maisha yao.
Aidha ametoa wito kwa waumini na wananchi kwa ujumla
kujitokeza kwa wingi kwa ajili ya kusherehekea maadhimisho hayo ya miaka kumi
na tano yatakayoanza mapema asubuhi nakutamatika jioni.
Kwa upande wake Mwenyekiti Bodi ya Afya wa Kituo cha Afya
Maji Matitu Bi.Hadija Hassan Ndende amewashukuru waumini hao kwa kujitoa kwa
kusaidia wakina mama wajawazito wenye mahitaji muhimu kwa kuwapatia msaada huo.
“Tunashukuru sana BCIC Majimeupe kwa kutuletea msaada huu
,sio mara ya kwanza kwenu kuja hapa,tunaomba muendelee na moyo wenu wa huruma
na mungu awazidishie maradufu ,tunaomba na taasisi zingine ziige kutoka kwenu
ili tuendelee kuwasaidia watu wenye uhitaji.
No comments
Post a Comment