Zinazobamba

DKT. NDUGULILE AJITOSA KUWANIA UKURUGENZI MKUU WHO KANDA YA AFRIKA,,RAIS DKT. SAMIA ABARIKI


Dkt. Faustine Ndugulile
NA Mussa Augustine

Serikali ya Tanzania imemtambulisha Dkt. Faustine Ndugulile kuwa mgombea wa nafasi ya Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) kwa ukanda wa Afrika katika awamu nyingine ya miaka kumi.

 Hayo yalisemwa Mei 8,2024 jijini Dar es Salaam na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mh.Januari Makamba wakati wa hafla ya utambulisho huo iliyohudhuriwa mabalozi wanaowakilisha nchi mbalimbali nchini, ambapo amempongeza Dkt. Ndugulile kwa kuidhinishwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwania nafasi hiyo itakayoleta heshima kwa Tanzania.

 Waziri Makamba amesema kuwa kutambulishwa kwa Dkt. Ndugulile ni ishara ya kufungua milango ya kampeni kuelekea kuwania nafasi hiyo muhimu inayobeba maslahi ya wananchi katika masuala mazima ya afya zao.

 "Dkt. Ndugulile ni mtu ambaye nimemfahamu kwa muda mrefu, ni mchapa kazi ambaye amebobea katika masuala ya afya, akihudumu katika nafasi mbalimbali Serikalini ikwemo Waziri wa Afya, na amefanya kazi na taasisi mbalimbali za kimataifa, hivyo ninaimani anafaa kuwa katika nafasi hiyo," amesema.

 Aidha meeleza kuwa hadi sasa wakati kampeni ya Dkt. Ndugulile ikizinduliwa ni kwamba ameshapata uungwaji mkono wa Jumuiya ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC).

 Nakuongeza kuwa” Uchaguzi utafanyika Mwezi wa nane Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo,hivyo tuna matumaini Makubwa Mgombea wetu wa mara ya kwanza kutoka nchini Tanzania atashinda katika kinyang’anyiro hicho.

Nae Waziri wa Afya Ummy Mwalimu amesema ni mara ya kwanza kwa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla kutoa mwakilishi wa kugombea nafasi ya Mkurugenzi wa WHO Kanda ya Afrika.

 "Mgombea wetu anauzoefu mkubwa katika masuala ya afya Duniani, hivyo hii ni nafasi sahihi kwa Dkt. Ndugulile,hivyo kutokana na ujuzi alionao Dkt. Ndugulile katika masuala ya Afya, anaamini atapeleka uzoefu mzuri WHO hususan katika utungaji na uboreshaji wa Sera za Afya kwenye Shirika hilo.”amesema Waziri Ummy.

Naye Dkt. Faustine Ndugulile ambaye nimgombea wa nafasi hiyo amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan  kwa kumuamini na kumpa kibali na kumuunga mkono katika kuwania nafasi hiyo.

 Dkt.Ndugulile amesema kuwa WHO kwa Kanda ya Afrika inasimamia nchi takribani 48, hivyo amesema kuwa miongoni mwa mambo atafanya akipata nafasi hiyo ni pamoja na kuendeleza mabadiliko katika shirika.

Hakuna maoni