Zinazobamba

TECNO WAZINDUA SIMU PHANTOM 8 DUBAI



Dubai, United Arab Emirates, October 22, 2017 – TECNO, Kampuni kubwa ya simu
 za mkononi TECNO iliyopo chini ya TRANSSION HOLDINGS , imetambulisha rasmi 
simu yake mpya  katika harakati zake za kukuza soko katika nchi za Asia na Africa, TECNO Phantom 8 katika jiji la Dubai. 
 Matumizi ya smartphone yanakua kwa kasi katika maeneo ya nchi za kiafrika na za mashariki ya kati kwa kiasi cha milioni 123. 7 mpaka 2016 toka milioni 106.4 mwaka 2015.
 “Hivi karibuni ripoti zinaonyesha kwa kiasi kampuni imeweza kupenya katika soko na kuleta 
ushindani  katika bara la Afrika na mashariki ya kati” Alisema makamu wa rais wa
 kampuni 
mama TRANSSION HOLDINGS, Arif Chowdhury. “Mipango yetu ni mwaka jana ilikua 
kukua zaidi kupitia mashariki ya kati hivyo kuzindua rasmi Phantom 8 jiijini Dubai 
ni hatua mojawapo 
katika kuendeleza mipango hii. Simu zetu zitaendelea kujikita katika kufuata mahitaji ya 
wateja zaidi”. Alimaliza Makamu wa raisi.
TECNO Mobile inaendelea kutoa bidhaa zenye ubora kwa wateja wake hasa barani 
Africa ambapo kampuni hiyo ina nafasi kubwa katika mauzo hasa kwa nchi kama 
Tanzania na Nigeria na nchi kadhaa kutokea mashariki ya kati.  

Kwa zaidi ya miaka 11 TECNO imekua ikifanya kazi ya kuunganisha wananchi katika mawasiliano kupitia simu hasa kwa kuleta simu zenye ubora na bei inayoendana
 na watumiaji wake.
Simu hiyo iliyozinduliwa jijini Dubai imekua gumzo tangu tetesi zitoke kua inakuja sokoni imezinduliwa ikiwa na jina la Phantom 8  huku ikiwa imetengenezwa kwa teknolojia kubwa hasa kwa upande wa kamera ikiwa na megapixel 20 mbele na kamera mbili 
nyuma6 GB RAM  na ROM ikiwa ni 64GB. Kwa upande wa dizaini simu 
inametengenezwa vizuri ikiwa na muundo wa mithili ya Almasi na kioo.
 Phantom 8 kutarajiwa kufika mabara mengine pia duniani.
Phantom 8 inauwezo wa kuweka “simcard” aina ya “Nano/ Micro” na inauwezo wa kumud memory card ya hadi 2TB (Terra Bytes) na pia inauwezo wa 4G plus
 ambayo inakuwezesha kutumia simu yako ndani na Zaidi ya nchi 200.
Kwa wateja waliopo Tanzania wataweza kuagiza simu hii mpya katika maduka maalumu ya simu za TECNO ili kuweza kuipata inapoingia sokoni siku chache zijazo. 
Phantom 8 iliyozinduliwa hivi karibuni iikiwa imesheheni na sifa za kipekee kama Kamera, Ubo na muonekano wa kipekee pamoja na kasi ya ajabu. Kamera ikiw ana uwezo wa 20 MP, 
pamoja na kamera pacha zenye uwezo wa 13Mp +12 Mp kamera za nyuma ikiambatana na uwezo wa kuvuta picha mara 10 zaidi ya kamera ya kawaida, Ina uwezo wa HDR,
4 in 1 uwezo wa kungarisha picha,AF na mambo mengine mengi yenye kukuhahkishia 
kupata picha zilizo bora na zenye muonekano mzuri.

Kwa maelezo zaidi kuhusian na TECNO Mobile tembelea https://www.tecno-mobile.com/index.php?m=Home&c=Index&a=index
###