NECTA YATANGAZA MATOKEO YA DARASA LA SABA LEO,SOMA HAPO KUJUA
BARAZA la Mitihani nchini (NECTA) limesema kiwango cha ufaulu katika mtihani wa darasa la saba uliofanyika Septemba 6 hadi 7 mwaka huu umeongezeka kwa asilimia 2.40 ukilinganisha na mwaka jana.
Hayo yamebainishwa leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa NECTA Dk. Charles Msonde akitangaza matokeo hayo, amesema watahiniwa 662,035 kati ya 909,950 waliofanya mtihani wamefaulu kwa kupata alama 100 au Zaidi kati ya alama 250.
Kati yao Wasichana ni 341,020 ambao ni sawa na asilimia 70.93 huku wavulana ni 321,015 sawa na asilimia 74.80.
Dk. Msonde amesema pia katika takwimu za matokeo zinaonyesha ufahulu katika masomo ya Kiswahili,Kiingereza na Hisabati umepanda kwa asilimia 4.25 ikilinganishwa na mwaka 2016.
“Watahiniwa wamefaulu Zaidi katika somo la Kiswahili ambapo ufaulu ni asilimia 86.86 na somo walilofaulu kwa kiwango cha chini Zaidi ni English Language lenye ufaulu wa asilimia 40.30,”amesema Dkt Msonde.
Hata hivyo Dk. Msonde ameiitaja mikoa iliyoongoza kitaifa ni Dar eSalaam,Geita,Kagera,Iringa,Kilimanjaro,Njombe, Arusha, Mwanza, Katavi, Tabora.
Kuhusu wanafunzi 10 bora kitaifa waliofanya vizuri kwenye mtihani huo ni Ibrahim Shaban kutoka Shule ya Tusiime iliyopo mkoani Dar es Salaam, Kadidi Mkama Kaddi kutoka shule ya Paradise iliyopo mkoani Geita,Mahir Ally Muhamed kutoka shule Feza iliyopo Mkoani Dar es Salaam,Mbarak Faraj kutoka shule hiyo hiyo ya Feza,
Dk, Msonde amewataja wengine waliofanya vizuri ni Philimon Damas kutoka shule ya St.Achileus iliyopo mkoani Kagera ,Huruma Godfrey kutoka shule Mwanga iliyopo Mkoani Kagera ,Hamza Azael Almas kutoka shule ya Azina iliyopo Mkoani Dar es Salaam,Gibbons Roy Fountain of Joy iliyopo Dar es Salaam,pamoja Erastus Joseph kutoka shule St Peter Claver iliyopo Mkoani Kagera.
Pamoja na hayo Dk Msonde Baraza hilo limetoa wito kwa Maafisa elimu wa Mkoa ,Halmashauri,Manispaa ,wadhibiti Ubora wa Elimu,wamiliki wa shule,Walimu wahakikishe ufundishaji na ujifunzaji unaimarishwa katika masomo yote shuleni ili kuwawezesha wanafunzi kupata umahiri unaotarajiwa.