Zinazobamba

SHEIKH WA MKOA: TUMUENZI IMAM KHOMEINI KWA KUKITHIRISHA UPENDO BAINA YETU, KIONGOZI WA KANISA APENDEZWA NA MATENDO YA KHOMEINI



Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa, amesema Imaam Khomeini anapaswa kuenziwa kwa vitendo hususani kuongeza jitihada za kupendana baina yetu, kuthamini wengne kwani kufanya hivyo kutasaidia kustawisha Amani iliyopo nchini. Pia amewasihi viongozi wa dini na vijana kujitoa kama  Imam Khomein (r.a) ambaye alijitoa kwa ajili ya watu wote ulimwenguni.

Wito huo ulitolewa jana Dar es Saalam wakati wa semina  iliyozungumzia mchango wa Imam Khomein (r.a) katika ulimwengu, ambayo iliyofanyika katika Masjid Ghadir, Kigogo Post Dar es Salaam.


Kiongozi mkuu wa Waislam Shia Ithna Asheriya Sheikh Hemed Jalala akiongea kwa msisitizo kuhusu umoja na msikamano kwa dini zote

Sheikh Alhad Mussa amesema Imam Khomein (r.a) alijitoa kwa ajili ya watu wote ulimwenguni, hakujitoa kwa ajili ya waislamu pekee, na wala hakujitoa kwa mashia pekee, bali amejitoa kwa kuhakikisha wanaadamu wanapata haki zao, wanyonge wanapata haki zao, na madhalimu hawana nafasi katika jamii.
Kingozi wa makanisa ya Ufunuo na uzima Tanzania Nabii Poul Bendera akiongea kwa niaba ya dini ya kikristo mapema leo jijini Dar es salaam
Kwa upande wake Muanzilishi na Kiongozi wa Kanisa la Ufunuo Tanzania Nabii Paulo Bendera ameema amejifunza mambo makuu matatu kutoka kwa Imam Khomein (r.a) ambayo ni uswa, haki na kuwatetea watu wanaonyonywa na wanaokandamizwa.

Imam Khomein alikuwa ni mtu wa watu, alikuwa anapenda haki, alikuwa anapenda usawa na alikuwa anawatetea watu wanaonyonywa pamoja na kuwatumikia watu kwadhati,

“Nashukuru sana kwasababu ninajifunza mengi ndani ya dini ya Kiislamu,hata miezi iliyopita nilimkaribisha sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Sheikh Alhad Mussa katika kanisani kwangu na nikampatia Ibada, ili ahutubie, waumini walifurahi sana,

Sisi Viogozi wa Dini tukiwa tunaonyesha ushirikiano baina yaViongozi wa Kikrito na Viongozi wa Kiislamu tunazidi kufungua nafasi zaidi ya Upendo, Mahusiano mema kati ya Udugu wa Wakristo na Waislamu

Nae Kiongozi Mkuu wa Waislamu Shia Ithnasheriya Tanzania Sheikh Hemed Jalala amesema kuwa Uislam unafunza kukaa vizuri na watu wote, unafunza huruma, unafunza amani na upendo kwa watu wote.

Aidha Sheikh Jalala amesema kuwa Uismau hauko dhidi ya asiyekuwa Mwislamu badi Uislamu upo dhidi ya Mtu yoyote amabe ni Dhalimu

Balozi wa Iran nchini Tanzania Mousa Farhang akiongea kwenye semina hiyo mapema jiji Dar es salaam