TFF YANGUKIA PUA MAHAKAMANI,KWENYE KESI YA MAAFISA WAKE,SOMA HAPO KUJUA
Mahakama ya hakimu mkazi Kisutu leo March 10 2017 imeripotiwa taarifa
ya mwisho kuhusu kesi iliyokuwa inawakabili watumishi wa shirikisho la
soka Tanzania TFF Juma Matandika ambaye ni msaidizi wa Rais wa TFF na
Martin Chacha ambaye alikuwa mkurugenzi wa mashindano.
Ilidaiwa kuwa Chacha na Matandika walinaswa kwa kurekodiwa sauti zao wakifanya mazungumzo na wanaotajwa kuwa ni viongozi wa Geita lakini leo baada ya Mahakama kujiridhishwa na uchunguzi imewaacha huru na kuona hawana kesi ya kujibu.
Martin Chacha
Maafisa hao wa zamani wa TFF wote wawili walikuwa wanatuhumiwa kwa kosa
la kuomba rushwa ya Tsh milioni 25 kutoka katika klabu ya daraja la
kwanza ya Geita Gold ili waisaidie kupanda Ligi Kuu kwa njia za ujanja
ikiwemo kupanga matokeo.
Juma Matandika
Ilidaiwa kuwa Chacha na Matandika walinaswa kwa kurekodiwa sauti zao wakifanya mazungumzo na wanaotajwa kuwa ni viongozi wa Geita lakini leo baada ya Mahakama kujiridhishwa na uchunguzi imewaacha huru na kuona hawana kesi ya kujibu.